Tuesday, June 05, 2012

TAYAMAMU

InshaALLAH Ukumbusho wetu Ujao Utakuwa unahusu Tayamamu Nini Maana ya Tayamamu na Sababu zipi ambazo Zina mfanya Mtu ku - Tayamamu Pamoja na Jinsi ya Kutayamamu kama kunavyoo nekana katika Picha.


InshaAllah waweza Fatilia Post zetu zaidi Katika Facebook : Kijana wa Kiislam Dsm


Au  katika Twitter :  Kijana wa Kiislam Dsm  au ukawasiliana nasi kwa Sms katika Namba : +255784199383


VIONGOZI

Mh Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr Jakaya Mrisho Kikwete akiwa katika Picha ya Pamoja na Mufti wa Tanzania Sheikh Issa Shaaban Simba .

Masheikh Zetu Tanzania


Sheikh Abuu- Bakar Zuber Mudiru wa Madrasatu Salafia  katika Moja ya Hafla Dar es Salaam.

Katika Picha anaoneka Prof: Juma Mikidadi , Sheikh Abdallah Sheikh Katika Moja ya Hafla Jijini Dar es Salaam.
                                         
             PICHA KWA HISANI YA KIJANA WA KIISLAM 

QUR AN TUKUFU



Maana ya Neno MUKALLAFU





Maana ya Neno MUKALLAFU

Hili neno huenda tukawa tunalitumia sana katika safari zetu za Ukumbusho wa FIQH unapokutana na Neno hili Jee tunakuwa na kusudio gani?

Ukikutana na Neno Mukallafu hukusudiwa katika Elimu ya Fiqh ni ule umri wa Baleghe ambao atakapofika mtu Mwanamume au
Mwanamke hupata sifa ya kuwa ni mtu MUKALLAFU.
Kwa Maana kwamba anatakiwa kuyatekeleza yale yote ambayo ameamrishwa na kukatazwa na sharia Mfano Swala, Funga na ibada nyingenezo.

NI WAJIB KWA MTU MUKKALAFU KUTENDA YOTE ALIYO AMRISHWA NA KUKATAZWA NA SHARIA ILA KUACHA KWA DHARURA.
MTU MUKKALAFU AKIFANYA MEMA NA KUACHA MABAYA KWA KUTII AMRI YA MOLA WAKE HUPATA THAWABU NA AKIFANYA MABAYA HUPATA DHAMBI.

DALILI ZA BALEGHE TATU.
1.Kutimiza Umri wa Miaka 15 kwa Mwanamke na Mwanaume.

2.Kuota kwa Mwanaume na Mwanamke anapofikisha Umri wa Miaka 9.

3.Kutokwa na Damu ya Hedhi kwa Mwanamke

Hizi ndio Alama Tatu pindi anapoziona Mtu au kwa Mtoto wake anatakiwa amuhimize sana ki - Ibada kwani kila tendo lake linakuwa linazingatiwa na Kuandikwa kama Jema Thawabu na kama Baya Dhambi.

Ni vyema kuwafundisha na kuwahimiza watoto wetu Mambo mema ya Kii baada na Malezi ya Ki - Dini na kuwaeleza wanapofika Umri huu kuwa sasa Tayari washaingia katika Umri ambao Sharia ya Dini Inawazimu kwao





Asalaam Alaykum Ndugu zangu wapendwa nawashukuru kwa kushiriki katika Swali tulilo Uliza Jee Ingekuwa Memory zetu (Akili) za kuhifadhi Zingekuwa GB 1 Nini ungeifadhi ?

MashaAllah wengi Mmejibu Majibu Mazuri sana Nimeyapenda Sana Na kutokana na Majibu yenu nimepata Nguvu ya Kuandika Ukumbusho Ufutao.

Ewe Ndugu yangu Mpendwa Miongoni mwa Neema ambazo M/Mungu ametupa sisi Wanaadamu Ni Akili ambayo inatutofautisha na Wanyama.

Na Neema Nyengine ambayo M/Mungu ametupa ni hii Open Memory ambayo haiko na Limit GB 1 wala GB 4 iko zaidi ya GB 8 Hivyo Ndugu zangu wapendwa Kwa vile Bado tuna Pumzi na Uhai Tuanze sasa hivi kwa Ku - Format na Ku - Scan Memory zetu kwa ajili ya Kuweka Mambo Mazuri katika Memory zetu kama vile tulivyo Chagua kwa GB1 wale waliochagua QUR AN & SUNNA na Mazuri mengi Muda Bado Upo ila tusichele kusema tutafanya Kesho kwa sababu kesho huenda tusifike Tuingize Elimu na yaliyo Mazuri katika Memory zetu ili kupata fikia Malengo yetu ya Kupata Radhi za M/Mungu na Kuishi Maisha Bora hapa Duniani na Kesho Akhera.

MASHAALLAH ALHAMDULLILAH KAKA YANGU HUYOOO NA DADA YANGU NAMUONA ANAFUTA KATIKA SIMU YAKE MIZIKI NA TAARABU NA KUTAFUTA QUR AN ILI ANZE KUWEKA MAZURI KATIKA MEMORY YAKE NA YA SIMU YAKE .

MUNGU AKUBARIKI KWA KUWA MTU WA MATENDO BAADA YA KUSIKIA MUNGU AWABARIKI NYOTE KWA KUWA NAMI

GB 1





Ndugu zangu Wapendwa hivi Ingekuwa Memory zetu (AKILI) za kuweza kuhifadhi vitu ni Gb 1 tu ambayo haina formatting wala Scanning kwa kuweka Data Mpya JEE WEWE UNGEPENDA KATIKA GB1 HIYO UHIFADHI NINI ?

Mambo ambayo Ni Haramu kufanya Mtu ambaye yupo katika hali hiyo ya Siku zake (HEDHI)





Ndugu zangu katika Imani Baada ya Kueleza Maana ya Hedhi na mengineyo InshaALLAH tunaendelea na kutaja Mambo ambayo Ni Haramu kufanya Mtu ambaye yupo katika hali hiyo ya Siku zake (HEDHI).

1.Kuswali

2.Kutufu Al-Kaaba

3.Kugusa Msaafu (Qur an)

4.Kuubeba Msaafu (Qur an)

Rejea Dalili ya Mwenye Janaba.

5.Kukaa msikitini

6.Kusoma Qur an

7.Kufunga Funga ya Faradhi au Sunna

Angalizo:-
Atalipa mwenye hedhi Funga iliyompita katika kipindi cha hedhi baada ya kusafika/Twaharika kwake.
Ama Kuhusu Swala hatakiwi kulipa zilizompita katika kipindi yupo katika Siku zake Mwanamke.

8.Kuachwa kwa Mwanamke (Kupewa Talaka )

9.Kupita Msikitini

Angalizo:-
Kupita msikitini kwa sababu damu ni najisi na ni haramu kuuchafua msikiti kwa najisi na uchafu mwingineo Ikiwa mwanamke atajiaminisha kutokuuchafua msikiti basi anaweza kukatiza na kupita msikitini.

10.Haifai Kuingiliwa kwa Maana kufanya naye tendo la ndoa Mwanamke ambaye yupo katika Siku zake

Dalili
M/Mungu anasema " BASI JITENGENI NA WANAWAKE WAKATI WA HEDHI (zao) WALA MSIWAKARIBIE MPAKA WATWAHARIKE. WAKISHAKUTWAHIRIKA BASI WAENDEENI
KATIKA PALE ALIPOKUAMRISHENI ALLAH…" Qur an Suratul Baqara Aya 222

Kusudio la kujitenga na wanawake ni kuacha kuingiliana nao kimwili.

Kwa Ibara Maarufu katika FIQH Madh hab haifai kwa Mwanamke aliye katika siku zake kustarehe Nae sehemu zilizo kati ya Kitovu na Magoti.
Tutakuwa tumefika Mwisho wa Ukumbusho unaohusu Hedhi Nipende kukumbusha Zaidi haya Ni Machache katika Mengi ambayo tunatakiwa tufahamu hivyo basi hii iwe Mwanzo na Chachu ya kusaka Walimu na Masheikh katika kutaka Jua / Uliza Mengi katika FIQH na Mambo ya Dini yote Tusitosheke na Post za Kijana Wa Kiislam Tuwe karibu Na Masheikh zetu tupate Tambua mengi TUTAENDELEA NA BAADHI YA MAREJEO YA NUKTA MUHIMU NAWASHUKURUNI

MAANA ISTIHAADHA





MAANA ISTIHAADHA

Istihaadha ni damu ya ugonjwa damu hii hutoka katika mshipa ulio ndani kabisa ya tumbo la uzazi.

Damu hii hutengua udhu lakini haiwajibishi josho kama ilivyo kwa
damu ya hedhi.
Vile vile damu hii haitoi fursa ya kuacha kuswali na kufunga.

Mwanamke mwenye maradhi haya ya Istihaadha anatakiwa aioshe damu na afunge utepe mahala itokapo kisha atawadha na halafu aswali.

Imepokelewa riwaya kutoka kwa Fatmah Bint Abiy Hubaysh M/Mungu amuwiye radhi kwamba yeye alikuwa akitokwa na istihaadha Mtume (S.A.W) akamwambia "Ikiwa ni damu ya hedhi, basi itakuwa ni damu nyeusi ijulikanayo.
Itakapokuwa hivyo basi acha kuswali, ikiwa ni nyingine basi Tawadha na uswali, hakika si vingenevyo huo ni mshipa ". Kama alivyosema Mtume imepokelewa Abu Daawoud.

NIFASI
Ama damu ya Nifasi Ni damu ambayo hutoka Baada ya Uzazi (Kujifungua).

Zote hizi Damu Mbili zitapo Mtokea Mtu zina Muwajibisha Kukoga Josho Kubwa (Josho la Faradh/Wajib ) tukisema Damu Mbili Nakusudia Hedhi na Nifasi ama Damu isiyo kuwa hiyo Rejea hapo Juu katika Kipengele cha Istihaadha.

ANGALIZO:-
Ziko Tabia za Baadhi ya watu Baada ya Kumaliza au kukata Damu ya Uzazi hutafuta Maalim kwa Ajili ya KumTwaharisha Hii si katika Dini ya Uislam Maelekezo ya Kukoga JOSHO KUBWA REJEA POST JINSI YA KUKOGA JANABA ILA KUNA BAADHI YA MAMBO MACHACHE HUENDA YA KAZIDI KATIKA HALI YA KUJISAFISHA SAIDIANENI WENYEWE KWA WENYEWE WANAWAKE WA KIISLAM KATIKA KUFUNDISHANA MEMA MNAPOKUTANA KATIKA SHUGHULI ZENU ZA WANAWAKE TU.

Ongezo katika Josho la Hedhi inapasa Misuko ya Nywele ifuliwe kutokana Josho hili linakuwa kwa Mwezi Mara Moja tu kwa Mwezi.

Ndugu zangu Mtaniwia Radhi lengo ni kukumbushana M/Mungu Ndiye Mjuzi.

MAANA YA HEDHI

Ndugu yangu katika Imani kama utakumbuka katika Post zilizopita tumetaja Mambo ambayo yanapo Mpata Mtu inamlazimu kukoga Josho la Waajib Faradh Alhamdullilah
tumeeleza Jambo Moja ambalo Ni Janaba Jinsi linavyo patikana na Jinsi ya Kujitwaharisha kwake InshaAlla leo tutaendelea na Baki ya Mambo mengine na tutazungumzia Hedhi Maana yake na Muda wake.

MAANA YA HEDHI

Neno Hedhi Ki Lugha Maana yake ni KUCHURIZIKA.

Kwa Mtazamo wa Watu wa Elimu ya Sharia ni DAMU YA MAUMBILE yaani damu hii ni
sehemu/ni katika jumla ya maumbile ya Mwanamke,
Mwanamke kaumbwa hivyo kwa lengo maalum.
Damu hii hutoka ndani kabisa ya tumbo la uzazi kila mwezi baada ya mwanamke kutimiza kwa uchache umri wa miaka tisa

DALILI
Dalili na ushahidi wa Kuwajibishwa Mwenye kutokwa Damu hiyo Kuji Twaharisha Kukoga Josho Kubwa.

Dalili katika Qur an M/Mungu anasema
"NA WANAKUULIZA JUU YA HEDHI , WAAMBIE HUO NI UCHAFU. BASI JITENGENI NA WANAWAKE WAKATI WA HEDHI (zao). WALA MSIWAKARIBIE MPAKA WATWAHARIKE.
WAKISHATWAHARIKA BASI WAENDEENI KATIKA PALE ALIPOKUAMRISHENI ALLAH…" Qur an Suratul Baqara Aya 222.

Dalili katika Sunna

Mtume(S.A.W) anasema Imepokelewa Hadith na Fatmah Bint Abiy Hubayshi M/Mungu amuwie Radhi Mtume anasema "Itapokujia hedhi , basi acha kuswali na itakapomalizika (kutoka) basi ikoshe damu (Twaharisha) na uswali"kama alivyosema Mtume Bukhaari na Muslim.

MUDA WA HEDHI

Kusudio la ibara (Muda wa hedhi) kipindi ambacho mwanamke hutumika
yaani huwamo hedhini.
Kipindi hiki tunaweza kukigawa katika sehemu tatu.

Kipindi kifupi
Kipindi kirefu
Kipindi cha katikati ( Ada )

KIPINDI KIFUPI

Huu ndio muda wa chini kabisa wa kutoka damu ya hedhi hiki ni kipindi cha masaa ishirini na nne (24).
Hii inaamaanisha kuwa mwanamke anaweza kuingia hedhini mchana na usiku wake tu kisha damu ikakatika.

KIPINDI KIREFU

Huu ndio muda wa juu kabisa wa kutoka damu ya hedhi
Hiki ni kipindi cha siku kumi na tano (15) mchana na usiku

KIPINDI CHA KATIKATI
Huu ndio muda wa ada na desturi kwa wanawake walio wengi, yaani wanawake wengi hutumika katika kipindi hiki. Huu ni muda wa siku sita au saba

Muda wa chini wa Twahara, yaani kipindi cha chini ambacho mwanamke anakuwa katika twahara ni siku kumi na tano(15).
Hakuna ukomo ( limit ) wa wingi wa Twahara kwani inawezakana kabisa mwanamkeasipate hedhi kwa muda wa mwaka miaka miwili au miaka kadhaa na hili limethibiti kwa majaribio

Mwanamke atakapoiona damu chini ya kipindi kifupi cha hedhi yaani chini ya masaa ishirini na nne au aliiona damu baada ya kule kipindi kirefu cha hedhi yaani baada ya siku kumi na tano, damu hii itazingatiwa kisharia kuwa ni damu ya ISTIHAADHA (Ugonjwa) na sio damu ya hedhi.

Hii Ndio Damu ya Hedhi ambayo Inamuwajibisha Kukoga Josho Kubwa Pale Inapo dhihiri kwake InshaAllah tuendelea kueleza Nini Istihaadha (Damu ya Ugonjwa ) na yanayo Pasa kwa Damu hiyo. M/Mungu Ndiye Mjuzi

Mambo ambayo Ni Haramu kwa Mtu Mwenye Janaba





Ndugu yangu Mpendwa katika Imani InshaAllah kwa uwezo wa Mungu Baada ya kuona Jinsi ya Kukoga Janaba kiukamilifu leo Tunaendelea na Post zetu kwa kuangalia Mambo ambayo Ni Haramu kwa Mtu Mwenye Janaba

1.Kuswali swala ya fardhi au ya sunna
Hii ni kwa mujibu wa kauli ya M/Mungu Mtukufu: "ENYI MLIOAMINI! MSIKARIBIE SWALA, HALI MMELEWA MPAKA MYAJUE MNAYOSEMA WALA HALI MNA JANABA ISIPOKUWA MMO SAFARINI ( mnapita njia ) MPAKA MKOGE…" Qur an Suratil Maidah Aya 43.

Maelezo ya Aya Kwa Ufupi Na Kusudio la Neno Swala.

Kusudio la neno SWALA katika aya hii ni MAHALA PA KUSWALIA ( msikiti ) kwa sababu kupita njia hakupatikani ndani ya Swala.
Ikiwa mwenye janaba anakatazwa kupita msikitini basi kukatazwa kuswali ni aula zaidi.
Ibn Umar Mungu amuwie Radhi amesema : Hakika nimemsikia Mtume (S.A.W) akisema " Haikubaliwi swala bila ya twahara".Kama alivyosema Mtume Hadithi Imepokelewa na Imam Muslim

Twahara iliyotajwa katika hadithi ni pamoja na Twahara ya hadath ndogo na Janaba ( hadathi kubwa ) Hadathi hii inafahamisha uharamu wa kuswali kwa mwenye hadath zote hizo hadathi ndogo na hadathi kubwa(Janaba).

2.Haifai kwa Mwenye Janaba Kutufu Al-Kaaba

3.Haifai kwa Mwenye Janaba Twawafu ya Nguzo/fardhi au ya sunna hii ni kwa sababu Twawafu iko katika daraja ya Swala kwa hiyo nayo imeshurutizwa Twahara kama ilivyo kwa Swala.

4. Kugusa Msaafu (Qur an )

5. Haifai kwa Mtu Mwenye Janaba Kuubeba Msaafu (Qur an )

6. Haifai kwa Mtu Mwenye Janaba Kukaa Msikitini

7. Kusoma Qur-ani. Amesema Mtume Muhammad (S.A.W) " Asisome mwenye hedhi wala mwenye janaba chochote katika Qur-ani".Kama alivyosema Mtume Imepokelewa na Tirmidhiy

ANGALIZO: INAFAA kwa mwenye Janaba kuisoma Qur an moyoni bila ya kuitamka kwa ulimi kama ambavyo inafaa kuutazama Msahafu bila ya kuushika vile vile Inafaa kusoma Dhikri/Nyiradi za Qur-an kwa kukusudia ile Dhikri na sio Qur an .
Mfano Dhikri ya Qur-ani ni kama kusema :-

"RABBANAA AATINAA FID-DUN-YAA HASANATAN WAFIL AAKHIRATI HASANATAN WAQINAA ADHAABAN-NAAR” Qur an Suratul Baqarah aya ya 201.
Kufaa huku kwa kusoma hii kwa Mtu Mwenye Janaba kwa kuikusudia aya hii kama dua na sio Qur an Mfano Mwengine anapopanda Kipando (chombo cha usafiri)
"SUB-HANNAL-LADHIY SAKHARA LANNA HAADHA WA MAA KUNNAA LAHU MUQRINIYN") Qur an Suratil Az- Zukhruf aya 13 kwa kuisudia hii kama dua na sio dhati ya Qur-ani yenyewe.
Mpaka Hapa Tutakuwa InshaAllah Tumefunga Kipengele cha Janaba Na InshaAllah Post ijayo Tutazungumzia Baaki ya Vitu Vingine ambavyo Vinampasa Mtu Kuoga Josho Kubwa Nawashukuruni Saana M/Mungu ndiye Mjuzi

Maana ya Nia





Maana ya Nia Ki Sharia ( FIQH )

NIA NI KUKUSUDIA KITU CHENYE KUAMBATANA NA KITENDO UNACHOTAKA KUTENDA ISIPOKUWA FUNGA.

Ikiwa Umenuia Kitu na hiko kitu ulichonuia kikawa hakikuambatana na Kitendo ambacho unataka kukifanya hiyo Inaitwa 3ZIMAA Na sio NIA.

MAHALA PA NIA NI MOYONI

Angalizo:-
Namba 3 Nakusudia Ayin = ع

NIA





Asalaam Alaykum Ndugu zangu wapendwa Katika Imani Natumai Mmeamka Salama
Wengi katika Ndugu walikuwa wanataka Dua ya Kukoga Janaba Naomba Kuanzia leo Tambua kuwa hiyo iliyokuwa unaijua kwa Jina la Dua inaitwa NIA kwa Ufasaha hakuna Dua ya kukoga Janaba wala Hedhi wala Nifasi Bali huitwa Nia ya Kukoga Ima JANABA HEDHI AU NIFASI.
Na Nia Zake huwa huwa kwa Maneno yafutayo na Sehemu ya Nia ni Moyoni.
NAWAYTU RAFAAL HADATHIL AKBAR.
NAWAYTU RAFAAL JANABA.
NAWAYTU RAFAAL HEIDHI
NAWAYTU RAFAA NNIFASI

ZOTE ZIKIWA NA MAANA NANUIA KUONDOSHA JOSHO KUBWA.

ANGALIZO:
Katika Somo lilopita tulielekeza Jinsi ya Kujitwahrisha na Josho la Janaba kwa Ukamilifu wengi wanauliza Vipi ukioga kwa Bomba la Mvua au Baharini N.k
Zingatia kupatikana Mambo matatu katika hali hizo na yakipatikana hayo Twahara yako Ni sahihi.
1.NIA
2.KUONDOSHA UCHAFU.
3.KUNEA MAJI MWILI MZIMA

YAKITIMIA HAYO BASI HAKUNA TATIZO LA KUJITWAHARISHA KWA NJIA HIZO

Jinsi ya Kukoga Janaba KIKAMILIFU


KARIBU INSHA ALLAH  M/MUNGU AKIPENDA TUTARUDI KATIKA 
KUENDELEZA GURUDUMU  LETU LA KUKUMBUSHANA KATIKA 
BLOG YETU.

WAKO.
GHALIB NASSOR MONERO 

AINA ZA JOSHO/KUKOGA , MAMBO YANAYOWAJIBISHA KUKOGA





Ewe Ndugu yangu katika Imani kama tulivyotangulia sema kuwa Inshallah Mara hii
tutaangalia AINA ZA JOSHO/KUKOGA , MAMBO YANAYOWAJIBISHA KUKOGA inshaAllah Tuanze Kuangalia.
AINA ZA JOSHO
Kuna Aina Mbili za Josho/Kukoga kwa Mtazamo wa FiQh

1.Faradhi/Wajib

2.Sunna

JOSHO LA FARADHI

Josho la Faradhi Ni Josho amabalo haitosihi Ibada yenye Kuitaji Twahara Mfano wa Swala Mpaka kukoga kwanza Pindi pale kutakapo kuwepo Sababu zake hilo Josho la Faradhi.

SABABU ZA JOSHO LA FARADHI/WAJIB
Sababu ambazo zinamfanya Mtu akoge Josho la Faradhi Ni Kama zifuatazo :-

1.Janaba.
2.Hedhi/Nifasi.
3.Kujifungua
4.Mauti

Haya Ndio Mambo ambayo yakimpata Muislam anatakiwa akoge Josho la Faradhi/Wajib.

Tuangalie Moja katika Mambo hayo Manne kwa Undani Japo Kidogo.

JANABA
Neno janaba linachukua maana ya MANII yatokayo kwa mchupo.
Tunaposema fulani ni mwenye janaba/ana janaba tunamaanisha si mwenye Twahara/hana Twahara kutokana na kutokwa na manii au kujamiiana yaani kutokana na kufanya tendo la ndoa.

MAMBO YASABABISHAYO JANABA :
Janaba husababishwa na mambo mawili
1.Mwanamume/Mwanamke kutokwa na manii.

2.Jimai

Njia Ambazo Mtu huweza kutokwa na Manii.

1.Kuota Usingizini kama anafanya Tendo la Ndoa
2.Kutoka Kwa Kuchezeana na kushikana shikana Baina ya Mwanamke na Mwanaume.
3.Kutoka kwa Athari za Kutazama/Kufikiri kuliko athiri Moyo N.k

2.Jimai
Katika Mambo ambayo yanasababisha Janaba ni Jimai Kwa Maana kujamiiana hata kama manii hayakutoka.
Mwanamume akiingiza sehemu tu ya Dhakari yake katika tupu ya mwanamke basi imewapasa wawili hao; mwanamume na mwanamke huyo kukoga josho la kisharia bila ya kuangalia wametokwa na manii au laa.

Kinachozingatiwa hapa ni muingiliano na mvaano wa tupu mbili hizo ya Mwanamume na Mwanamke na si utokaji wa manii.

Dalili.
Imepokelewa na Abu Hurayra Radhi za M/Mungu zimshukie Juu yake kutoka kwa Mtume (S.A.w) amesema : " Mwanamume akikaa baina ya mapaja na miundi yake (mwanamke), halafu akamuendesha mbio, hakika limekwishapasa josho" kama alivyosema Mtume Bukhari na Muslim.

Na katika upokezi wa Imaam Muslim kuna ziada " Hata kama hakutokwa na manii". Kama alivyosema Mtume.

Maana ya Manii kwa Pande Zote Mbili Mwanaume na Mwanamke Manii kwa upande wa mwanamume ni maji Meupe, mazito yachupayo ambayo hutoka wakati anapofikia kilele cha matamanio ( Hutoka kwa Ladhaa Utamu ).

Manii Upande wa Mwanamke ni maji ya manjano na ni mepesi.

Ziko Hadithi Nyingi Zinazo tolea dalili kuwa utokaji wa manii huwajibisha josho Miongoni Mwazo ni Imepokelewa na Ummu Salama M/Mungu amuwie radhi amesema : Ummu Sulaym alikuja kwa Mtume (S.A.W) Akasema : Ewe Mtume wa M/Mungu, bila shaka M/Mungu haoni haya kusema haki, jee, inampasa mwanamke kuoga atakapo ota ? Mtume akajibu : " Naam , atakapo yaona maji (manii)" Kama alivyosema Mtume Bukhari na Muslim.

MAANA YA JOSHO





Asalaam Alaykum Ndugu zangu katika Imani leo kwa Uwezo wake M/Mungu Tupo katika Kuangalia Maudhui Mpya Katika Mlango huu huu wa Twahara ambao Tumeuanza Mawiki yaliyopita InshaAllah Tuendelea Kujikumbusha Machache ambayo yanahusu Josho/Kukoga kwa Kadri M/Mungu atakavyo tuwezesha Tuanze Kuangalia Maana ya JOSHO/KUKOGA katika Sharia.

MAANA YA JOSHO

Josho kisharia ni kitendo cha kuyapitisha/Sambaza maji mwili mzima kwa nia maalum.

HUKUMU NA DALILI YA JOSHO
Josho kisharia ni WAJIBU/FARDHI kwa Kila Muislam pale atakapo patwa na Moja katika Mambo ambayo yanamlazimu Kukoga Mfano Janaba,hedhi na Nifasi.

Dalili ya Kupasa Kukoga/Josho Qur an Sunna
Dalili ya Kwanza Qur an .
M/Mungu Mtukufu anasema "NA MKIWA NA JANABA BASI OGENI" Qur an Suratul Maidah Aya ya 6.
Na amesema tena katika Aya Nyengine "NA WANAKUULIZA JUU YA HEDHI; WAAMBIE HUO NI UCHAFU. BASI JITENGENI NA WANAWAKE WAKATI WA HEDHI ( Siku zao ). WALA MSIWAKARIBIE MPAKA WATWAHIRIKE" Qur an Suratul - Baqara aya ya 222.

Dalili katika Sunna
hadithi iliyopopkelewa na Abu Hurayra Radhi za M/Mungu Zimshukie Juu yake amesema, Amesema Mtume wa M/Mungu rehma za Mungu zimshukie Juu yake na Amani "Ni haki ya kila muislam kukoga siku moja katika jumaa, akaosha kichwa na mwili wake" Bukhari na Muslim.

HEKMA YA KUKOGA/JOSHO.

1.Kupata Thawabu
Kwa sababu josho kwa maana na mtazamo wa kisharia ni IBADA kwa kuwa ndani yake kuna kutekeleza amri ya sharia na kuitumia hukumu ya sharia Kwa hivyo kwa utekelezaji huu wa amri na hukumu ya sharia Mja hupata ujira Mkubwa kwa Mola wake.
Rejea Hadith ya Bwana Mtume Muhammad (S.A.W) Anasema "Twahara ni nusu ya imani" Kama alivyosema Mtume Imepolewa Hadith na Imamu Muslim.
kwa Mujibu wa Hdithi hiyo Ni vyema ikaeleweka kuwa Twahara imekusanya Udhu, Josho, Tayamam Na N.k.

2.Kuwa Msafi Muislam anapokoga mwili wake hutakasika na kuwa msafi. Usafi huu ni kinga kubwa ya vijidudu vinavyoweza kusababisha maradhi kama vile upele na N.k.

3.Kuwa Mchangamfu na kupata nguvu Mpya.

Hizi ni katika Hekma za Chache za Kukoga/Josho ama Kwa Ujumla tunaweza sema kuwa falsafa ya josho Twahara vitu hivi humuandaa Mtu/Mja na kumuweka katika nafasi nzuri ya kuwasiliana na kuzungumza na Mola Muumba/Mola wake ndani ya swala akiwa katika hali njema kabisa.

InshaAllah Post Ijayo Tutaangalia AINA ZA JOSHO Mambo ambayo yanamuwajibisha Mtu kukoga na Ukamilifu wa Kukoga M/Mungu Ndiye Mjuzi

NDOA





Arguments and misunderstandings are going to happen even in the best of marriages. Good communication and calmly listening to each other’s views can remove tensions and problems.
If you are going through difficulties and sincerely want to ...make your marriage work, make Dua and don’t give up! Allah SWT said “…if the both of them truly desire reconciliation, Allah will bring about a reconciliation between them ” Qur an An Nisa Verse Number 35.

َإِنْ خِفْتُمْ شِقَاقَ بَيْنِهِمَا فَابْعَثُوا حَكَماً مِنْ أَهْلِهِ وَحَكَماً مِنْ أَهْلِهَا إِنْ يُرِيدَا إِصْلاحاً يُوَفِّقْ اللَّهُ بَيْنَهُمَا إِنَّ اللَّهَ كَانَ عَلِيماً خَبِيراً

Tafsiri ya Aya ya Surat An Nisa Aya Namba 35. M/Mungu anasema " Na mkichelea kutakuwapo mfarakano baina ya mke na mume basi pelekeni muamuzi kutokana na jamaa za mume, na muamuzi kutokana na jamaa za mke. Wakitaka mapatano Mwenyezi Mungu atawawezesha. Hakika Mwenyezi Mungu ni Mjuzi Mwenye habari. "

Hii Ndio Njia Kuu ya Marejeo Pale WanaNdoa wanapo Patwa Na Jambo katika Maisha yao ya Ndo Sio Kukimbilia Polisi. 

SEHEMU AMBAZO SUNNA KUWA NA UDHU





Ndugu yangu katika Imani baada ya Kuona yale yaliyo Haramu kwa Mtu asiyekuwa na Udhu InshaAllah Tuangalie baadhi ya Hali ambazo UDHU HUSUNIWA NDANI YAKE.

1.Wakati wa kumtaja (dhukuru) Mwenyezi Mungu Mtukufu
Kumbuka Ewe Kijana Mwenzangu wa Kiislam kuwa Udhu ni silaha ya muumini ni vyema saa zote ukawa unatembea na silaha yako na hasa wakati wa kumtaja (dhukuru) M/Mungu.

2.Wakati wa kulala.
Dalili Hadithi Albaraai bin Aazib Radhi za M/Mungu zimshukie Juu yake amesema : Aliniambia Mtume (S.A.W) "Unapo kiendea kitanda chako (unapotaka kulala) Tawadha udhu wako wa swala kisha ulalie upande wa kulia halafu useme : ALLAHUMMA INNIY ASLAMTU NAFSIY ILAYKA, WAWAJJAHTU WAJ-HIY ILAYKA, WAFAWWADHTU AMRIY ILAYKA, WA AL JA-TU DHWAH RIY ILAYKA RAGHBATAN WA RAHBATAN ILAYKA, LAA MALJAA WALAA MANJAA MINKA ILLAA ILAYKA. ALLAHUMMA AAMANTU BIKITABIKAL-LADHIY ANZALTA, WABINABIYYIKAL-LADHIY ARSALTA." Kama alivyosema Mtume Bukhari.
3.Ni Sunna kutia udhu kabla ya kukoga josho la janaba.

4.Wakati mtu anapokuwa na Hasira sana, ni sunna akatawadhe kwa sababu udhu husaidia kuzima mchemko wa hasira na humrejesha katika hali ya utulivu.

Haya Ni baadhi ya Mambo ambayo ni Sunna Kuchukuwa Udhu kabla ya Kuyafanya yako Mengi sana Ni juu yetu Mimi na wewe Kijana wa Kiislam kuwa Karibu na Wajuzi wa Mambo ili tupate wauliza na kufahamu zaidi ya Baki ya Mambo Mengine.

Mwisho Tumalize UDHU WA MWENYE UDHURU

Tunakusudia Udhu wa watu ambao wana maradhi ambayo kwa Maradhi hayo wawezi kuhifadhi udhu wao kama wanavyoweza watu wengine katika hali ya kawaida.
Hawa ni kama wale ambao wenye Maradhi ya kutoweza kuzuia haja Ndogo (Mkojo) au mwanamke ambaye hutokwa na Damu ya Ugonywa Ukiacha Damu ya Hedhi ya kila mwezi.

Hukumu ya udhu wa watu hawa ni kwamba wanatakiwa watawadhe kila unapoingia wakati wa kila swala, wasitawadhe kabla ya kuingia wakati kwa kuwa wanatakiwa kufululiza baina ya udhu na swala.
Hii ni kwa sababu kisharia hawana udhu kwani wana hadathi ya kudumu na udhu wao ni wa ruhsa maalum waliyopewa na sharia ili waweze kuyatekeleza yale yote yasiyo tekelezeka bila ya udhu, kama vile Swala N.k
Udhu wa watu hawa utabatilika na kutenguka mara tu unapoingia wakati wa swala nyingine.
Akitaka kuswali basi itamlazimu kutawadha tena. Haya yote yanaonyesha wepesi wa sharia ya Kiislamu ambayo imejengwa juu ya misingi ya wepesi na kuondosha uzito na ugumu.

Amesema M/Mungu Mtukufu : "Wala hakuweka juu yenu mambo mazito katika Dini. Nayo ni mila ya baba yenu Ibrahim …" Qur an Surat Al - Haj Aya ya 78.
Mpaka hapo Ndugu yangu tutakuwa Tumemalize Ukumbusho wetu Kuhusu Udhu Inshallah Ukumbusho Ujao utakuwa Unahusu Jinsi Ku - Jitwaharisha na Josho Kubwa yaani Jinsi ya Kukoga Janaba NAWASHUKURUNI WOTE

DUA YA KULALA





Ewe Kijana Mwenzangu Ni Sunna Ukiwa Unaelekea Kulala Kuchukua Udhu na Kusema Maneno yafutayo :-

ALLAHUMMA INNIY ASLAMTU NAFSIY ILAYKA, WAWAJJAHTU WAJ-HIY ILAYKA, WAFAWWADHTU AMRIY ILAYKA, WA AL JA-TU DHWAH RIY ILAYKA RAGHBATAN WA RAHBATAN ILAYKA, LAA MALJAA WALAA MANJAA MINKA ILLAA ILAYKA. ALLAHUMMA AAMANTU BIKITABIKAL-LADHIY ANZALTA, WABINABIYYIKAL-LADHIY ARSALTA LAA ILLAH ILLA ALLAH MUHAMMMADU RASUL ALLAH.
Na Unapolala LALA KWA UPANDE WAKO WA KULIA Shukrani

MAMBO YALIYO HARAMU KWA ASIYE NA UDHU




Ndugu zangu Katika Imani Baada ya Kuona Vitenguzi vya Udhu Inshallah Leo kwa Uwezo wake M/Mungu tunaangalia
MAMBO YALIYO HARAMU KWA ASIYE NA UDHU

Ni haramu kisharia kwa mtu asiyekuwa na udhu kufanya mambo yafuatayo : -

1.Kuswali swala ya aina yeyote ya faradhi, au sunna au swala ya maiti Unamlazimu Udhu kwanza Ndio apate kutekeleza Ibada hizi.
Dalili.
M/Mungu anasema "ENYI MLIOAMINI ! MNAPOTAKA KUSWALI, BASI OSHENI NYUSO ZENU, …" Qur an Suratil Maidah aya ya 6.
Dalili katika Sunna.
Mtume(S.A.W) anasema " Mwenyezi Mungu haikubali swala ya mmoja wenu atakapo huduthi mpaka atawadhe (tena)" kama alivyosema Mtume hadith imepokelewa na Imamu Bukhaar.
Kumbuka Ewe kijana Mwenzangu kuwa Twahara ya hadathi ni sharti miongoni mwa sharti za kusihi Swala haitosihi Swala ila kwa kupatikana Twahara ambayo ni udhu.

2.Kutufu/kuizunguka Al-Kaaba.

3.Kuugusa Msahafu wote au baadhi yake.
Wamekubalina na kuwafikiana wanazuoni wa fani hii ya fiqh kwamba INAJUZU kwa mtu asiyekuwa na udhu kuisoma Qur-ani Tukufu bila ya KUIGUSA lakini ni Bora kwake kuwa na Udhu.
Kama alivyo ruhusiwa mtoto mdogo kuigusa bila ya udhu kwa lengo la kujifunza, kwa kuwa yeye si MTU MUKALLAF ( anayelazimiwa na hukumu za sharia).
Pamoja na ruhsa hii bado ni bora azoweshwe kuigusa Qur-an Tukufu akiwa na udhu ili kuipandikiza heshima na utukufu wa Qur-ani ndani ya moyo wake huyu kijana na achipukie akijua nini Maana ya Twahara na Ubora wake akuwe akitofautisha kati ya Qur ani na vitabu vingine.
Ndugu yangu katika Imani haya ni Machache katika tuliyojaaliwa na M/Mungu kwa Upana zaidi wa Mas alaa (Elimu hii ya Fiqh Nakushauri Kuwa Karibu Na Masheikh na Maustaadh wa Dini Ili wapate kukupa Faida zaidi M/Mungu ndiye Mjuzi zaidi

VITENGUZI VYA UDHU




VITENGUZI VYA UDHU

Ni mambo ambayo mojawapo miongoni mwake likimtokea/kumpata mtu mwenye udhu litasababisha kubatilika kwa udhu wake huo na kuhesabika mbele ya sharia kuwa hana Udhu.
Itampasa kuchukua Udhu tena ikiwa anataka kuyafanya yale ambayo kisharia hawezi kuyafanya Pasina Udhu.

Vitenguzi vya udhu ni vitano

1.Kutokwa na Kitu kati ya Moja ya Njia Mbili ya mbele au ya nyuma. Ni sawa sawa hicho kilichomtoka ni haja Ndogo au Kubwa au Upepo.
Dalili katika Qur an : -
M/Mungu anasema “…..AU MMOJA WENU AMETOKA CHOONI."Qur an Surat Maida Aya ya Sita,[Surat An Nisaa aya ya 43.
Maana yaani ametoka kukidhi haja yake.

Dalili katika Sunna :-
Mtume (S.A.W) “ Allah haikubali swala ya mmoja wenu atakapo huduthi ( atakapotengukwa na udhu ) mpaka atawadhe ( tena ) Mtu mmoja wa Hadharamout (Mji katika Yemen ) akasema kumuliza Abuu Hurayrah ni nini hadathi? akamjibu ni ushuzi(upepo) ".Kama alivyosema Mtume.

Madhii na Madii ni Katika Vitenguzi vya Udhu.
Rejea Somo letu katika Post za Nyuma tulipotaja Aina za Najisi.

TANBIIH : Kisia/kadiria kwa haya yaliyotangulia kila kitokacho katika tupu ya mbele au nyuma, hata ni twahara kilichotoka.

2.Kulala Usingizi Mzito hali ya kutoambatanisha Makalio katika Aridhi kiasi cha kuruhusu chochote kuweza kumtoka bila kuhisi hasa ushuzi (Upepo).
Dalili kutoka katika Sunna kauli ya Mtume – (S.A.W) “Atakayelala ( akiamka ) basi na akatawadhe” Kama alivyosema Mtume Imepokelewa na Abuu Daawoud
Ama ule usingizi mwepesi ambao mtu anakuwa anazo hisia zake na akawa amekaa mkao wa kuwambisha makalio yake katika ardhi, huu hautengui udhu kwa sababu atahisi kitakachomtoka.

3.Kuondokewa/kutokwa na akili kwa sababu ya uwendawazimu, kuzimia, kulewa ( kwa namna yoyote ile ) au kwa kutumia madawa ya kulevyaii ni kwa sababu vitu hivi huiondosha akili ya binadamu na hivyo kumfanya akose hisia za kuweza kutambua kinachomtokea.

4.Kumgusa Mwanamke(Si mtoto Mdogo) wa kando pasina kizuizi, Mwanamke wa kando ni kila Mwanamke ambaye kisharia ni halali kumuoa, hakuna uharamu baina yao ima wa Ki Nasabu/Kunyonya au Ukwe .
Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu “….AU MMEWAGUSA WANAWAKE…”Qur an Suratil An Nisa aya 43

TANBIIH
Udhu hutenguka kwa Wote wawili aliyegusa na aliyeguswa.

5.Kugusa utupu wake au wa mtu mwingine hata kama ni mtoto mdogo au maiti kwa matumbo ya kiganja chake au matumbo ya vidole vyake pasina kizuizi.
Dalili juu ya hili ni kauli ya Bwana Mtume (S.A.W) “Atakayeigusa dhakari yake, basi asiswali mpaka akatawadhe (tena)”Kama alivyosema Mtume imepokelewa na Tirmidhiy.


Hivi Ndugu zangu katika Imani Ndio Vitenguzi vya Udhu naomba Nikumbushe Ukumbusho wangu Umetegemea katika FIQH YA IMAMU SHAFII yako Mambo wametofautina wanawachuoni Niwaombe tuchukue tu kama ilivyo na Inshallah Katika Safari yetu M/Mungu akitupa Umri tutaeleza Mambo yote ambayo yako na tofauti katika FIQH MUQAARANA M/Mungu ndiye Mjuzi Ndugu yenu katika Imani

YALIYO KARAHA KATIKA UDHU





Ndugu katika Imani Baada ya Kueleza Sharti za kusihi Udhu Inshallah yapo Mambo ni karaha kufanya kwa MTU mwenye kuchukua Udhu Baadhi ya Mambo hayo ni :-

YALIYO KARAHA KATIKA UDHU

1.Ni karaha kwa mwenye kutawadha kuacha sunna yeyote miongoni mwa sunna za Udhu tulizozitaja kwa sababu kuacha kuzitekeleza suna hizo kutampelekea mtu huyo kukosa Thawabu, na muislam wa kweli siku zote hupupia kuitekeleza ibada yake kwa ukamilifu na kwa namna ilivyofundishwa na mwenyewe Bwana Mtume (S.A.W)

2.Ni karaha kuyatumia maji kwa israfu (fujo)

3.Ni karaha kutanguliza kuosha mkono/mguu wa kushoto kabla ya mkono/mguu wa kulia , kwa kuwa kufanya hivyo ni kinyume na alivyotenda Bwana Mtume (S.A.W).

4.Ni karaha kukausha/kufuta viungo vya udhu kwa kutumia leso/taulo.
Ukaraha huo utaondoka kwa udhuru kama vile baridi kali, hapo itakuwa si karaha.

5.Ni karaha mtu kuoshwa viungo na mtu mwingine bila ya kuwa na udhuru ukubalikao kama ugonjwa.
Hili limefanywa kuwa ni karaha na sharia kwa sababu ndani yake mna aina ya kibri na ubwana, vitu ambavyo Uislam Unavipinga.

6.Ni karaha kwa aliyefunga kuyapeleka ndani sana maji katika kusukutuwa na kupandisha maji puani.
Hii ni kwa sababu ya kuchelea kufika Maji kooni na kusababisha kuharibika Funga yake.
Amesema Mtume (S.A.W) “ Na balighisha ( yapeleke maji ndani sana ) katika kupandisha maji puani , ila ukiwa umefunga ( usibalighishe )” Kama alivyosema Mtume Imepokelewa na Abuu Daawoud.

TANBIIH : Ikiwa imekatazwa kubalighisha katika kupandisha maji puani kwa mfungaji, basi kubalighisha katika kusukutua ni bora zaidi kukatazwa.

Inshallah Post ifuatayo itakuwa Vitenguzi vya Udhu kwa Uwezo wake Allah

Sharti za kusihi udhu





Ndugu zangu katika Imani Baada ya Kueleza Sunna za Udhu leo kwa Uwezo wake Allah Tunaendelea kueleza Sharti za Kusihii huo Udhu.

Sharti za kusihi udhu
Maana yake ni mambo ambayo mwenye kutawadha aya hakikishe kwanza kabla hajaanza kutawadha, ili udhu wake uweze kusihi na kukubalika kisharia. Miongoni mwa sharti muhimu kabisa za udhu ni kama zifuatazo :

1.Kutokuwepo kizuizi kinachoweza kuzuia maji wakati wa kutawadha kuuifikia ngozi, Mfano wa Kizuizi kama mafuta mazito ya mgando, ute wa mshumaa, rangi ya lami, na vitu vyenye kufanana.

2.Lisimpate mwenye kutawadha wakati wa kutawadha kwake jambo lenye kuubatilisha na kuutengua udhu wake, kama vile kutokwa na kitu katika mojawapo wa tupu mbili.

3.Maji ya udhu yawe ni TWAHARA na yenye kufaa kutumika kwenye udhu.

4.Kutakata mwanamke kutokana na damu ya hedhi na nifasi, kwani udhu hausihi wala kumpasa mwanamke aliye katika hedhi au nifasi mpaka atakapotahirika.

5.Uislamu wa mwenye kutawadha, kwani udhu si wajibu na wala hausihi kwa asiyekuwa muislamu, hata kama atafata taratibu zote za udhu.

6.Kusiku wepo juu ya kiungo cha udhu kitu chochote kinachoweza kuharibu mojawapo ya sifa tatu za maji, ambazo ni tamu (ladha), rangi na harufu. Vitu hivi ni pamoja na vumbi la mkaa, chokaa, Cement N.k

Hizi Ndizo Sharti za Kusihi Udhu.
Maelezo zaidi kuhusu Sharti ya 6 Uislam Ndiyo Nguzo ya Kwanza katika Kusihi Ibada zote Iwe Swala, Funga , Hijja na Nyenginezo katika Ibada hazitosihii ibada ya Funga na tulizozitaja kwa Mtu asiyekuwa Muislam hata kama atakuwa anafunga Sharti la Uislam Lizingatiwe ili kupata kusihi kwa Ibada yake.
Mpaka hapo Ndugu yangu Tutakuwa tunaenda sawa na Inshallah Tuzidishe Maombi na Ibada katika Mwezi huu wa Rajaab kuelekea Shaaban na kufikia Mwezi Mtukufu wa Ramadhan Maandalizi Bora Ni Kujikurubusha zaidi kwa Mungu na Kumuomba M/Mungu kufika katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhan Haya Ndio Mapokezi Sahihi ya Mja mwema

DUA





JIANDAE NA MWEZI MTUKUFU WA RAMADAN KWA KUOMBA DUA HII AMBAYO WAJAA WEMA NDIO WANAYOITUMIA KATIKA KUMUOMBA MUNGU.

Ewe M/Mungu Tupe Baraka za Mwezi wa Rajab Na Shaaban , Na Tunakuomba M/Mungu Tufikishe tukiwa wazima wa Afya katika Mwezi Mtukufu wa Ramadan ili Tutekeleze Ibada ya Funga.

O Allah, bless ( the month of ) Rajab for us, and allow us to experience Ramadan this year.

اللهم بارك لنا في رجب وشعبان وبلغنا رمضان

ALLAHUMA BAARIK LANA FII RAJAB WA SHAABAN WABALAGHNA RAMADHAN

O Allah , ALHAMDULLILLAH FOR EVERYTHING





Say Alhamdullillah When you sit with your Family , As There Is Someone Somewhere Wishing to have.

Say Alhamdullillah when you Go to work , As Many People Are Still Lookin For a Job.

Say Alhamdullillah Because You are Healthy , As The Sick Ones Wish To Buy Health No Matter How High The Price Is.

Say Alhamdullillah Because You are Still Alive , As The Dead Would wish To come Back to life To Do Good Deeds.

Say Alhamdullillah Because You Worship Allah , As Other Worship Idols and Money.

O Allah , ALHAMDULLILLAH FOR EVERYTHING
O Allah , ALHAMDULLILLAH FOR EVERYTHING
O Allah , ALHAMDULLILLAH FOR EVERYTHING
O Allah , ALHAMDULLILLAH FOR EVERYTHING

SUNNA ZA UDHU


SUNNA ZA UDHU
Maana ya sunna katika elimu ya Fiqh ni NJIA iliyopokewa kutoka kwa Mtume kwa maneno au vitendo.

Sunna kifiqh zimegawanyika sehemu mbili

1.Suna Muakkadah (Suna kokotezwa)
2.zisizo Muakkadah (Suna zisizokokotezwa)

Suna Muakkadah
Ni zile alizodumu nazo Bwana Mtume (S.A.W) kuzitenda na hakuziacha ila kwa udhuru
mkubwa sana.

Hukumu yake
Hukumu ya suna muakkadah ni kulipwa thawabu mtendaji na kulaumiwa na sheria mwenye kuacha kuitenda.

Sunna zisizo muakkadah
Ni zile ambazo Bwana Mtume(S.A.W) alizitenda baadhi ya wakati na kuziacha wakati
mwingine.

Hukumu yake.
Hukumu ya suna hii ni kulipwa thawabu mtendaji na wala haadhibiwi mwenye kuacha
kuzitenda.

Sunna zisizo Muakkadah huitwa Majina Mengine MANDUBU au MUSTAHABBU.

SUNNA ZA UDHU.

1.Kupiga Bismillah mwanzoni mwa kutawadha. Imepokelewa kutoka kwa Swahaba Anas Mtume (S.A.W) amesema "Tawadheni kwa BISMILLAH" yaani semeni hivyo mnapoanza kutawadha kama alivyosema Mtume. Nasaai

2.Kukosha vitanga vya mikono kabla ya kuviingiza chomboni ikiwa anatawadha kwa kutumia chombo mfano wa kopo.

3.Kupiga Mswaki :
Hili linatokana na kauli ya Bwana Mtume (S.A.w) Lau si kuwaonea uzito umati wangu,
ningeliwaamrisha kupiga mswaki pamoja na kila udhu" kama alivyosema Mtume Bukhar na Muslim.

4 na 5.
Kusukutua na kupandisha maji puani kwa kutumia mkono wa kulia na kisha kumeka kwa kutumia mkono wa kushoto.

6.Kuasua ndevu nyingi, yaani kuzichokoa ili maji yaweze kupenya ndani ya ngozi.

7.Kupaka maji kichwa chote/kizima.

8.Kusafisha sehemu zilizo baina ya vidole vya mikono na miguu.

9.Kupakaza masikio maji, nje na ndani kwa majimapya sio yale yaliyotumika katika kupakaza kichwa.

10.Kuosha na kupakaza maji viungo mara tatu tatu.

11.Kuanza kuosha mkono/mguu wa kulia kabla ya mkono/mguu wa kushoto.

12.Kusugua, huku ni kupitisha mkono juu ya kiungo wakati wa kukiosha.

13.Kufululiza, yaani kuviosha viungo kwa kufuatanisha kimoja baada ya kingine pasi na
kutia mwanya kati yake, kiasi cha kutokauka kiungo cha mwanzo kabla ya kuoshwa kiungo cha pili. Kufanya hivi ni kumfuata Bwana Mtume, kwani hivi ndivyo alivotawadha.

14.Kurefusha kuosha mipaka/sehemu za uso, mikono na miguu.

15.Kutofanya israfu katika utumiaji wa maji,ikawa mtu anayamwaga majo ovyo ovyo. Ni muhimu tukakumbuka kwamba maji ni miongoni mwa neema kubwa kabisa alizoneemeshwa nazo binadamu, kwani maji ni uhai. Kwa mantiki
hii ni vema tukayatumia kwa uangalifu, ikiwa ni pamoja na kuvihifadhi vyanzo vya
maji.Tujiepushe na matumizi mabaya ya maji katika kila shughuli/kazi za maisha yetu ya kila siku, hasa hasa katika kutawadha na kukoga.

16.Kuelekea Qiblah wakati wa kutawadha kwani huo ndio upande mtukufu kuliko pande zote.

17.Kutokuzungumza wakati wa kutawadha. Haya yote ni kumfuata Bwana Mtume (S.A.W)

18.Kuomba/Kuleta dua hii baada ya kumaliza kutawadha, elekea Qiblah na sema :
DUA BAADA YA UDHU.
(ASH-HADU AN LAA ILAAHA ILLAL-LAAHU WAHDAHU LAA SHARIYKA LAHUU, WA ASH-HADU ANNA MUHAMMADAN ‘ABDUHUU WARASUULUH, ALLAHUMMA JA3LNIY MINAT-TAWWABIYNA, WAJA3LNIY MINAL-MUTATWAHHIRIYN, WAJA3LNIY MIN ‘IBAADIKASWAALIHIYN, SUBHAANAKALLAHUMMA WABIHAMDIKA, ASH-HADU AN-LAA ILAAHA ILLA ANTA ASTAGHFIRUKA WA ATUUBU ILAYKA).

Hapa Inshallah Tutakuwa tumefikia Mwisho wa Mlango wa Sunna Tunamuomba M/Mungu atudumishe katika kufuata Faradhi zake na kushikamana na Sunna Za Mtume (S.A.W) ili kupata Radhi za M/Mungu Ewe Mungu Tusaidie waja wako

Nguzo za Udhu





Nguzo za Udhu

Kusudio la neno Nguzo hapa ni yale mambo ambayo ni lazima kupatikana ili kutimia UDHU wako likikosekana au kupungua moja miongoni mwao, udhu huwa ni batili kisharia.Zifuatazo Ndio Nguzo za Udhu kwa Utaratibu Kama tulivyoelekezwa katika Qur an na kufasiriwa na Mtume Muhammad (S.A.W)
Nguzo za Udhu ziko Sita 6.

1.NIA
Hii ndio nguzo ya kwanza ya udhu.
Neno “nia” Maana yake katika lugha ya kawaida ni MAKUSUDIO.
Ama katika Sharia na watu wa Fiqh ni MAKUSUDIO YA KITU/JAMBO HALI YA KUAMBATANISHA KITU/JAMBO HILO NA KITENDO CHAKE.
na Nia hukaa moyoni mwa mtu. Dalili ya ufaradhi nia Hadith ya Mtume (S.A.W) “Hakika (kusihi kwa) amali kumefungamana na nia na kila mtu (atalipwa) kwa mujibu wa nia (yake).." Kama alivyosema Mtume Hadith imepokewa na Imam Bukhar na Muslim

Malengo ya Nia katika Udhu.
Ni kupambanua baina ya ibada na ada na Udhu ni Ibada .Mfano mwengine wa kumbanua kati ya Ada na Ibada Mfano wa Kukoga kuna kukoga kwa kujisafisha na kukoga kwa Ajili ya kuondosha Josho kubwa Sasa Nia ndio itakayo tofautisha kati ya Mawili hayo Ada au Ibada.Basi kwa mantiki hii ikawa ni lazima udhu uambatane na nia.
Namna ya nia ni mtu kusema moyoni mwake :

“Nawaytu Fardhal-udhui” au
“Nawaytu Raf-al Hadath” au
“Nawaytu istibahat-swalaat”

Muda wa Kuleta Nia katika Udhu.
Nia huletwa wakati wa kuosha fungu/sehemu ya mwanzo ya uso, kwa kuwa hapo ndio mwanzo wa udhu yaani udhu unaanzia hapo na yaletwayo kabla ya hapo huhesabika kama maandalizi ya kuingia ndani ya udhu.

2.Nguzo ya Pili katika Nguzo za Udhu KUOSHA USO MZIMA/WOTE
Dalili kauli ya M/Mungu Mtukufu “BASI OSHENI NYUSO ZENU …”Qur an Suratil Maidah Aya ya 6

Kuosha uso mzima ndio nguzo ya pili ya udhu. Uso huoshwa mara moja tu kwa kuitegemea kauli ya Mtume : “Udhu ni mara moja moja”. Ama kule kuosha mara ya pili na ya tatu ni sunna. Imethibiti riwaya kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu –Rehema na Amani zimshukie – alitawadha mara moja moja na akasema : “Huu ndio udhu ambao Allah haikubali swala ila kwao” Na akatawadha (tena) mara mbili mbili na akasema : “Huu ndio wa wa mtu ambaye Allah atampa ujira mara mbili” Na akatawadha (tena) mara tatu tatu na akasema : “Huu ndio udhu wangu na udhu wa mitume kabla yangu, basi atakayezidisha (zaidi ya) hivi au kupunguza, (huyo atakuwa) amechupa mipaka na kufanya dhuluma”

Mipaka ya Uso
Uso katika Udhu huanzia maoteo/mameleo ya nywele za kichwa mpaka chini ya kidevu, huo ni urefu Upana wake ni tokea ndewe moja ya sikio hadi nyingine. Eneo lote lililo katika mipaka hiyo, ndio huitwa uso katika sharia. Na ni wajibu kuosha kila kilichoota ndani ya mipaka hiyo kama nyusi, kope, sharubu na ndevu.
Ndevu huoshwa nje na ndani zikiwa chache. Ama zikiwa ni nyingi zilizoshindamana kiasi cha kutokuona ngozi basi inatosha kuosha juu yake tu.

3.KUOSHA MIKONO HADI VIFUNDONI
Imelazimu maji yaenee vema katika nywele na ngozi. Ukiwepo uchafu chini ya kucha ukayazuiliya maji kupenya ndani au pete iliyobana isiyoruhusu kupenya maji, udhu hautasihi bali utakuwa ni batili.

4.KUPAKAZA MAJI SEHEMU YA KICHWA
Jinsi Mtume alivyokuwa akipaka za Kichwa imepokelewa na Abdallah ibn Zayd Mtume (S.A.W) Alipakaza (maji) kichwa chake kwa mikono yake, akaipeleka mbele halafu akairudisha nyuma, alianzia sehemu ya mbele ya kichwa chake kisha akaipeleka kichogoni, kisha akairudisha pale mahala alipoanzia”

5.KUOSHA MGUU HADI VIFUNDONI
Inampasa mwenye kutawadha ahakikishe anaosha sehemu yote iliyoainishwa katika sheria. Asiache sehemu yeyote ile iliyo chini ya kucha.

6.MPANGO/TARATIBU.
Kufuatilizisha baina ya viungo hivi vinne vya udhu kwa namna ilivyokuja ndani ya Qur-ani Tukufu.
Na dalili ya Nguzo hii ya Sita inapatikana katika Kauli yake Mwenyezi Mungu Mtukufu aliposema katika Qur an : “ENYI MLIOAMINI! MNAPOTAKA KUSWALI, BASI OSHENI NYUSO ZENU NA MIKONO YENU MPAKA VIFUNDONI, NA MPAKE (maji) VICHWA VYENU, NA (osheni) MIGUU YENU MPAKA VIFUNDONI”Qur an Surat Maidah Aya ya 6.

Ewe Ndugu yangu katika Imani haya Mambo sita NDIO Nguzo za Udhu.
Inshallah tuwe makini sana katika kuchukua kwetu Udhu kwani Tukumbuke kwamba kubatilika kwa Udhu kunapelekea kubatilika Swala kwakuwa Udhu Ndio Msingi kuu wa Swala

NAMNA YA KUCHUKUA UDHU


Ewe Ndugu yangu katika Imani Kama tulivyosema kuwa Ukumbusho Ujao utakuwa ni namna ya kuchukua Udhu baada ya kuona Maana ya Udhu, Hukmu za Udhu na Dalili zake,Ubora na Fadhila za Udhu naonelea ni Bora tuuishi katika hii hii Siku ya Ijumaa kwa Kuangalia 
NAMNA YA KUCHUKUA UDHU kutokana na Umuhimu wa Udhu katika Maisha yetu ya kila Siku ya Ibada .

1.NAMNA YA KUCHUKUA UDHU
Ikiwa unachukua Udhu kwa kutumia chombo kama vile birika/Kopo basi ni vyema kama inawezekana liwe upande wako wa kulia na kama unatumia bomba basi fungua bomba lako na fuata Hatua zituatazo:

1.Anza kukosha vitanga vya mikono huku ukisema BISMILLAHIR-RAHMANIR-RAHIYM. Mara 3.

2.Baada ya kuosha vitanga vya Mikono, tia maji mdomoni na Sukutua mara 3.

3.Pandisha maji puani na safisha tundu za Pua mara 3

4.Osha uso wako ukianzia Kuanzia maoteo/mameleo ya nywele za kichwa mpaka mwisho wa kidevu kwa urefu na toka ndewe moja ya sikio hadi nyingine kwa upana.

Angalizo

Pindi unapokuwa unakosha ndio sehemu ambayo unatakiwa ulete/tia Nia na Mahala pake Moyoni ama kuitamka Nia ni Sunna kama tulivyoelekezwa na walimu wetu katika Fiqh.
Matamshi ya Nia Ni kama yafutayo :
NAWAYTU RA-AL HADATH (Nanuia kuondosha Hadathi/uchafu)
au
NAWAYTU FARDHAL-WUDHU(Nanuia kutekeleza Wajibu wa Udhu) au maneno yenye kufanana na hayo ma pia Uso huoshwa mara 3.

5.Kuosha mikono Miwili ukianzia mkono wa kulia kisha Mkono wa kushoto. kumbuka kuwa na Mikono Nayo Huoshwa mara 3.

6. Kupaka Maji sehemu katika Kichwa Mara 3.

7.Kukosha masikio , ndani na nje mara 3.

8.Ni hatua ya Mwisho nayo ni kuosha Miguu ukianzia wa kulia kisha wa kushoto Mara 3.

Kwa utaratibu huu udhu wako utakuwa umekamilika na hivyo kumaanisha kuwa sasa unayo rukhsa ya kusimama na kuzungumza na M/Mungu ndani ya swala.
Ewe Ndugu yangu Mpendwa katika Imani kumbuka kuufuta Utaratibu huu kwa Namba kama tulivyo elekeza ili kuenda kama alivyotuelekeza Mtume(S.A.W) kutoka kwa Maswahaba zake
Inshallah Nina Imani Mpaka Hapa Utakuwa umepata Muangaza fulani katika Uchukuaji wa Udhu Inshallah Ukumbusho unaofuata utahusu Nguzo za Udhu

UDHU




Ndugu yangu katika Imani Kaka yangu Mpendwa Dada yangu Mpendwa leo Inshallah kwa Uwezo wake M/Mungu Mtukufu tunaingia katika Ukumbusho Mpya Niwaombe wale Marafiki zetu na Ndugu zetu wageni warejee katika Post zetu zilizotangulia ili tupate kwenda sawa.Ukumbusho wetu leo utahusu au zungumzia Udhu na Kama Ada yetu tunaangalia neno kwa Maana Mbili ya Lugha na Maana ya watu Sharia(Fiqh).

1.MAANA YA UDHU

Tamko/Neno udhu linafasirika katika lugha ya kiarabu kama wema, uzuri na ung'avu.
Ama maana ya udhu katika istilahi ya wanazuoni wa fani hii ya Elimu ya Sharia (Fiqh) Udhu ni twahara inayotumia maji, twahara hii inahusisha viungo maalum vya mwili, baadhi yake hukoshwa kama mikono, uso na miguu na vingine hupakwa maji kama vile kichwa.

2.HUKUMU YA UDHU NA DALILI YAKE
Udhu kwa maana tulivyoieleza ni FARDHI/WAJIBU katika kusihi na kukubalika kwa ibada ya swala kwani hapana swala bila ya udhu kwa maneno mengine, tunaweza sema kuwa udhu ndio msingi mkuu na imara wa ibada ya swala.
Udhu ndani ya Qur-ani unapatikana katika kauli ya Mwenyezi Mungu aliposema :
"Enyi mlio amini! Mnapo simama kwa ajili ya Swala basi osheni nyuso zenu, na mikono yenu mpaka vifundoni, na mpake vichwa vyenu, na osheni miguu yenu mpaka vifundoni..." Qur an Suratil Maidah aya ya 6

Ama dalili na ushahidi wa udhu katika sunna ni ile kauli yake Mtume wa Mwenyezi Mungu Rehma za M/MUNGU zimshukie Juu yake na amani aliposema " Allah haikubali swala ya mmoja wenu atakapohuduthi kwa Maana kwamba atakapo tengukiwa na udhu mpaka atawadhe (tena)" kama alivyosema Mtume
Hadithi imepokelewa na Maimamu wawili.

3.UBORA/FADHILA ZA UDHU
Ewe Ndugu yangu Kijana Mwenzangu tukumbuke kwamba zimepokelewa hadithi nyingi kutoka kwa Bwana Mtume -Rehema za M/Mungu zimshukie juu yake na Amani katika kutaja na kuonyesha ubora na fadhila za udhu miongoni mwa hadithi hizo ni :-
Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu Rehema na Amani zimshukie juu yake "yeyote atakaye tawadha vyema ( kama alivyoelekezwa na sharia), hutoka madhambi zake mwilini mpaka chini ya kucha zake"kama alivyosema Bwana
Mtume Muslim.
Na katika Hadithi Nyengine Mtume (S.A.W)
amesema "Hakika umati wangu wataitwa siku ya Kiyama (mbele ya Mola wao) hali ya kuwa wang'avu wa nyuso, mikono na miguu kutokana na athari ya udhu, basi yeyote yule awezaye kurefusha mipaka ya viungo vyake (katika kutawadha) na afanye hivyo." kama alivyosema Mtume Imepokelewa Hadith na Imamu Muslim.

Ewe Ndugu yangu Mpendwa baada ya kujua haya
Inshallah azimia na tia Nia kuanzia sasa kushikamana na Udhu ili zisikupite fadhila na Ubora wa Udhu kama tulivyo eleza Inshallah tuwe pamoja katika Ukumbusho Ujao ambao tutaeleza Namna ya kutawadha.

KUSTANJI NA ADABU ZAKE




Ewe Kijana Mwenzangu katika Kumbusho Muhimu sana Ni zote zilizopita na hii tuifanyie kazi Mungu Tusaidie na tupe uwezo katika kutekeleza Maamrisho yako Amiin
Ukumbusho wa leo Unahusu Kustanji.

Maana yake
Kustanji/Kuchamba ni kusafisha na kuondoa najisi iliyotoka katika mojawapo ya tupu mbili Mbele au Nyuma ya Mwanaadamu.

Kustanji/Kuchamba baada ya kukidhi haja ni WAJIBU/FARADHI kama tutakavyoona katika kauli za Mtume Muhammad Rehma za M/Mungu zimshukie juu yake na amani.

Ina faa Kustanji kwa kutumia Maji Mutlaq(maji halisi) ambayo ndiyo asili katika kujitwahirisha na najisi.

Inajuzu pale panapokuwa hakuna Maji kutumia vitu vyenye Sifa zifuatazo:-
1.Kigumu Mf wa Jiwe.
2.Chenye Kuparuza (kisichoteleza)
3.Kinachoweza kuondosha najisi.

Kumbuka kwamba katika vyote hivyo ni bora kutumia Maji na kama uko na vyote viliwili uanze kisichokuwa Maji kisha umalizie na Maji kwani Huondosha Najisi yote kinyume na Vingine.

Ni haramu kustanji kwa kilicho chakula cha binadamu kama vile mkate au chakula cha majini kama vile mifupa. Amesema Bwana Mtume Rehma za Mungu zimshukie Juu yake na amani Amesema " Msistanji kwa (kutumia) kinyesi cha wanyama wala mifupa kwani hiyo (mifupa) ni chakula cha ndugu zenu majini" kama alivyosema Mtume Imepokelewa hadith na Tirmidhiy.


ADABU/TARATIBU ZENYE KUFUNGAMANA NA UINGIAJI NA UTOKAJI MAHALA PA KUKIDHI HAJA


Ni Vema kwa mwenye kutaka kukidhi haja, atangulize mguu wake wa kushoto wakati wa kuingia chooni na mguu wa kulia wakati wa kutoka chooni, kama tulivyofundishwa na Mtume wa Mwenyezi Mungu. Kadhalika asiingie na chochote chenye jina la Mwenyezi Mungu au jina lolote tukufu kama vile jina la Mtume au aya ya Qurani Tukufu. Bali imemlazimu muislamu kukivua kitu hicho wakati wa kuingia chooni. Pia imesuniwa kuleta dua wakati wa kuingia chooni. Pia imesuniwa kuleta dua zilizothibiti kutoka kwa Bwana Mtume kabla na baada ya kutoka chooni.

Aseme anapoingia Chooni

BISMILLAH ALLAHUMMA INNIY AUDHUBIKA MINAL KHUBUTHI WAL-KHABAITH.

Na anapotoka aseme :-
aseme
GHUFRAANAKA AL-HAMDU LILLAHIL-LADHIY ADH-HABA ANNIYL-ADHA WA-A’AFANIY.



ADABU/TARATIBU ZINAZOFUNGAMANA NA MAHALA PA KUKIDHIA HAJA

1.Njia ya watu au mahala wanapokaa, hii ni kutokana na kero na maudhi yatakayowapata.

2.Tundu iliyopo ardhini au ufa wa ukuta/kiambaza. Hii ni kwa sababu ya kumlinda na kumuepusha mkidhi haja na madhara yanayoweza kumpata. Kwani anaweza akawamo ndani ya shimo/ufa mdudu mwenye kudhuru kama vile nge au nyoka, huyu akakerwa na haja akaamua kumtokea mtu na kumdhuru
3.Chini ya mti utoao matunda.
Hii ni kwa ajili ya kuyahifadhi na kuyalinda matunda yado ndokayo yasipatwe na najisi.
Ni mamoja ikiwa matunda hayo yanaliwa au hayaliwi lakini yana manufaa mengine kama dawa.Na Miti ya Kivuli kwa ajili ya Mapumziko ya watu kwa uchovu na ukali wa jua.

4.Maji yaliyotuama (yasiokwenda). Hii ni kutokana na kichefuchefu watumiaji wa maji hayo yakiwa ni mengi yasiyoharibika na najisi na kuyanajisi yakiwa machache na hivyo kuyafanya yasifae kutumika.

Imekuwa ni kawaida kwa watu kukidhi haja sehemu yeyote bila ya kuchunga Adabu hizi huenda tulikuwa hatufahamu Leo Inshallah tumefahamu tujilinde ndugu zangu na Najisi na tuzilinde sehemu zetu katika kuweka Mazingira Safi Uislam Ni Usafi Ni aibu na haifai kwa Muislam kwenda kinyume na Misingi ya Mafundisho yako.M/Mungu ndiye Mjuzi zaidi Inshallah Mungu akipenda tutaendelea ...

Say Alhamdulillah





My Dear Brothers and Sisters In Islam

Say Alhamdulillah.
Alhamdulillah...Who returns me my soul back....Alhamdulillah Who gives me health...Alahamdulillah Who gives me the one more day and one more chance to seek His forgivness...Alhamdulillah Who reminds me to praise and thank Him while many of people don't.......PLEASE say ALHAMDULILLAH for everything...Wish you all a happy and blessed day




Ewe Ndugu yangu katika Imani Inshallah kwa uwezo wake Allah tunahitimisha Ukumbusho wetu wa Mlango wa Najisi na jinsi ya kutwaharisha kwake kwa kumalizia vitu vya aina Mbili ambavyo ukumbusho uliopita hatukuviongelea nanvyo ni
SAMLI, JIBINI, SIAGI NA MFANO WA VITU HIVYO PAMOJA JINSI YA KUITWAHARISHA NGOZI.

1.SAMLI, JIBINI, SIAGI NA MFANO WA VITU HIVYO

Samli, jibini siagi na vitu vinavyofanana navyo vikiingiwa na najisi na vikiwa katika hali ya ugumu yaani vimeganda na haviko katika hali ya kumiminika,
hutwahirika kwa kuitoa najisi iliyoingia pamoja na sehemu zinazozunguka zilizo jirani na najisi ile.

Bwana Mtume Rehma za M/Mungu zimshukie juu yake na Amani aliulizwa kuhusiana na (hukmu ya) panya aliyetumbukia (na kufia) ndani ya samli, akajibu "Mtupeni na sehemu inayomzunguka na kuleni samli yenu". kama alivyosema Mtume Imepokewa Imamu Bukhar
Ewe Ndugu yangu katika Imani ama ikiwa Samli, Siagi, Jibini na chochote chenye kufanana navyo katika hali ya kumiminika/maji maji na ikaingiwa na najisi ita najisika yote na haitofaa tena kwa matumizi ya binadamu.


2.TWAHARA YA NGOZI

Ngozi ya mnyama hutwahirishwa kwa kudibaghiwa.
Dabgh ni kuondosha damu, mafuta na mabaki ya nyama zilizosalia katika ngozi baada ya mnyama kuchunwa.
Uondoshaji huu hufanyika kwa kutumia vitu vikali vyenye muonjo wa asidi au Jivu, baada ya hapo ndipo ngozi hutwahirishwa na maji na kufaa kutumika kwa matumizi mbali mbali ya binadamu.
Imepokelewa na Ibn Abbas – Mungu amuwie Radhii Bwana Mtume (S.A.W) Amesema "Ngozi itakapo dibaghiwa imetwahirika" kama alivyosema Mtume Imepokewa Hadith na Maimamu wawili Bukhaar na Muslim.
TANBIHI
Haitwahariki Ngozi ya Nguruwe,Mbwa na viwili vinavyo zaliwa na wawili hao
Hapo InshaAllah Tutakuwa tumemaliza/tumehitimisha ukumbusho wetu inshallah tujiandae na Maudhui Mpya

MWENYE KUIHAMA QUR AN





Ewe Ndugu yangu katika Imani Kijana Mwenzangu M/Mungu anasema :-

Na (yeyote) atakaye jiepusha na mawaidha yangu, basi kwa yakini atapata maisha yenye dhiki, na Siku ya Kiyama tutamfufua hali ya kuwa kipofu.
Aseme:(huyo mtu atakae fufuliwa kipofu) Ewe Mola wangu Mlezi! Mbona
umenifufua kipofu, nami nilikuwa nikiona?(Mwenyezi Mungu) atasema: Ndivyo vivyo
hivyo. Zilikufikia ishara(Aya) zetu, nawe ukazisahau; na kadhaalika(vilevile) leo unasahauliwa.
Qur an Surat Taha Aya 124 Mpaka 126.

Subhana Allah
Takafakarii Ndugu yangu Natambua kwamba kuwa mbali na Allah hata kama utakuwa Taajiri Milionea basi utakuwa bado upo katika Maisha ya Dhiki na Mwisho wake kama Qur an ilivyoeleza Mungu tusaidie waja wako tusiwe mbali na Maamrisho yako.

Hii picha nimeipata katika moja ya website ambapo walikuwa wakieleza Utukufu wa Qur an Wadudu wameweza tafuna pembeni ya Ma s hafu na wameheshimu kuyafikia maneno yake Allah Subhanahu wa Taa3la.
Ndugu zangu tujitahidi tusiihame Qur an kiasi hiki