Sunday, August 18, 2013

M/MUNGU MTUKUFU  NI MWEMA ANAKUBALI KILICHO CHEMA TU.
Kutoka kwa Abu Hurayra Radhi za M/Mungu zimshukie Juu yake na Amani   amesema:  Amesema Mtume  Rehma za M/Mungu zimshukie Juu yake na Amani,
M/Mungu Mtukufu ni Mwema na anakubali kilicho chema tu.(hakubali kisicho chema au kizuri). 
Na Hakika ya M/Mungu Mtukufu ameamrisha Waislamu kufanya yale aliyowaamrisha Mitume,    amesema  M/Mungu Mtukufu "Enyi Mitume Kuleni katika vitu vyema na mfanye yaliyo sawa" .   M/Mungu Mtukufu amesema :" Enyi mlioamini kuleni katika vitu vyema ambavyo tumekuruzukuni” Kisha akataja (kisa cha yule) mtu aliyesafiri safari ndefu, kachafuka na kajaa mavumbi na huku anayanyua mikono yake mbinguni akisema "Ewe    Mola! Ewe Mola! Nipe kadhaa, nikinge na kadhaa wakati chakula chake cha haramu, na kinywaji chake ni cha haramu, na kivazi chake ni cha haramu, na    anashibishwa na haramu, je, vipi atajibiwa (dua zake?).
  Hadithi Imepokelewa na Imamu Muslim

No comments:

Post a Comment