Sunday, August 11, 2013

MUENDELEZO MPYA  WA MKASA WA SHEIKH ISSA PONDA

Assalam Alaykum
Ndugu Waislamu na Wote Wapenda Amani

Napenda kuwapa up-date ya Mtihani wa Sheikh wetu, Ponda Issa Ponda

Mchana huu amepelekwa Hospitali moja ya Jijini Dar es Salaam kwa matibabu zaidi (maana risasi bado iko mwilini)

Jina la Hospitali litatajwa jioni ya leo Katika Msikiti wa Mtambani, in Shaa Allah

Anaejua jina hilo anaombwa ASILITAJE MPAKA MUDA HUO ili watu wasiiende Hospitali kabla ya kuhudhuria Kongamano la Alaasisiri ya leo (soma chini)

PIA,

Ndugu Waislamu MNAOMBWA LEO SAA 10.00 ALAASIRI MUHUDHURIE KONGAMANO KUBWA litakalofanyika Katika Msikiti wa Mtambani, Kinondoni, Dar es Salaam, mara tu baada ya Swala ya Alaasir (saa 10.15 jioni)

Vile vile mnaombwa kutuma taarifa hii kwa email na kutumia sms ili wengi wahudhurie kwa wingi

Zaidi ya hayo, tuongeze Dua kwa Sheikh Ponda na Familia yake katika kipindi hiki kigumu zaidi

___________________________________________________________

Shura ya Maimamu chini ya Sheikh Kundecha Musa Kundecha imeitaka serikali kuunda tume huru kufanya uchunguzi kuhusu kadhia ya kujeruhiwa kwa Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu nchini, Sheikh Ponda Issa Ponda.
Sheikh Ponda


Katika mkutano wake na waandishi wa habari katika Msikiti wa Mtambani jijini Dar es Salaam, Amiri Kundecha aliyeongozana na wakili wa Sheikh Ponda, Bwana Nassoro Juma, ameitahadharisha serikali kuwa inaelekea kupoteza imani yake kwa wananchi, hususan Waislamu, kutokana na dalili zote kuonesha kuwa polisi ndio waliohusika na tukio hilo.
 

Jeraha alilopata


Tamko  hili pia Limeungwa mkono na Baraza kuu la Waislamu Tanzania Bakwata la kuundwa tume huru ya Uchunguzi wa tukio hili hayo yamesemwa na Sheikh Alhad Mussa Salum Sheikh wa Mkoa wa Dar es salaam kwa Niaba ya Mufti wa Tanzania katika kUPINGA KITENDO KILICHOTOKEA KWANI JESHI LA POLISI LILIKUWA NA UWEZO WA KUMKAMATA NA KUFIKISHA KATIKA VYOMBO VYA SHERIA,

No comments:

Post a Comment