Funga ya Sita ni Sunna inayopatikana katika Mwezi huu wa Shawaal baada ya Kumaliza Mwezi Mtukufu wa Ramadhani Mtume (S.A.W) Rehma za M/Mungu zimshukie Juu yake na Amani anasema "Atakeyefunga
Mwezi wa Ramadhani kisha akafuatilia (kufunga) siku
sita katika mwezi wa Shawaal (anakuwa)
kama
aliyefunga maisha yake yote,”
Na hii ni kwa
sababu mtu anapofunga mwezi mmoja wa Ramadhani, anapata thawabu ya kufunga
miezi kumi, kwa sababu mtu anapotenda Jema moja hulipwa kumi badala yake. Na
anapofunga siku sita katika Shawwal, anakuwa mfano wa
aliyefunga siku sitini. Ukijumlisha funga ya Ramadhani na
funga ya sita, unapata miezi kumi na miwili, na kwa ajili hiyo anakuwa mfano
wa aliyefunga mwaka mzima. Na mtu anapoendelea hivyo
maisha yake yote anakuwa mfano wa
anayefunga maisha yake yote”.
NAMNA YA KUFUNGA.
Imam Annawawi
ambae ni katika Maulamaa wakubwa wa madhehebu ya
Imam Shafi anasema;
"Ni vizuri
kufunga siku sita mfululizo mara tu baada ya kumalizika sikukuu ya mwanzo, na
atakayefunga siku sita mbali mbali katika mwezi wa Shawaal
, pia inakubaliwa”.
Amma
Imam Ahmed bin Hanbal anasema;
“Ukifunga mfululizo au ukizifunga siku sita tofauti katika mwezi
wa Shawaal yote ni sawa tu.”
UZINDUZI.
Maulamaa wanasema kuwa;
‘Lazima mtu atimize Ramadhani yake
kwanza, ndiyo aweze kufunga sita. Yaani ikiwa mtu anadaiwa
katika Ramadhani, basi lazima alipe kwanza deni
lake
lote
kisha ndio afunge sita.’
Na hii
ni tafsiri ya kauli ya Mtume (S.A.W) Rehma za M/Mungu zimshukie Juu yake na Amani aliposema;
“ATAKAYEFUNGA Mwezi wa Ramadhani KISHA akafuatilia (kufunga) siku sita…”
Wakasema kuwa kutokana na
kauli hii, Mtume (S.A.W) Rehma za M/Mungu zimshukie Juu yake na Amani hapa anasisitiza kuwa mtu lazima kwanza afunge Mwezi wa
Ramadhani, KISHA afunge sita. Na ikiwa mtu ana deni la kufunga, basi huyo
anakuwa hakufunga mwezi wa Ramadhani, na kwa ajili
hiyo ikiwa anazitaka thawabu zilizotajwa katika hadithi hiyo, basi inampasa
kulipa deni lake kwanza, kisha ndiyo afunge sita.
No comments:
Post a Comment