Saturday, August 10, 2013

AZHAR SHAREEF KILA PEMBE YA DUNIA

 Mwalimu Mkuu wa Markazi Islamiyah - Changombe akiongea na Waumini wa Kiislam katika Swala ya Eid , Mnazi Mmoja Dar es salaam  , Jana.
Sheikh wa Mkoa wa Dar es salaam akisalimina na Baadhi ya Waumini baada ya kumaliza Swala ya Eid.

Azhar Shareef ni Miongoni mwa Vyuo vikubwa duniani ambavyo vina historia ndefu sana katika Malezi ya Elimu ya Dini.

Azhar Shareef Makao Makuu yake yapo  Cairo , Misri na Miongoni mwa harakati zake ni kupeleka Walimu/Wahadhiri katika Nchi mbalimbali za Afrika na Ulaya.
Ofisi za Makao makuu ya Azhar.


Tawi la Azhar Shareef kwa nchini Tanzania lipo Changombe ( Barabara ya Uwanja wa Taifa) vile vile yapo Matawi madogo katika  Mikoa ya Arusha na Iringa.

Tawi hili la Azhar Nchini Tanzania hutoa nafasi za Masomo ya Juu kwa baadhi ya Wanafunzi ( kuwapeleka Nchini Misri) ili kujiendeleza zaidi .

Mpaka leo wametoa Vijana wengi sana Na Masheikh wengi Tanzania Miongoni Mwao ni Marehemu Sheikh Suleiman Gorogosi
, Sheikh Muhidin Hassan , Sheikh Yahya Mkali n.k 

Kuna Changamoto kubwa sana Vijana wanaomaliza chuo Nchini Misri wanaporudi nyumbani kujiunga Moja kwa moja katika kazi za Daahwa kwa kukosa viunganishi kutokana na Maisha ya nyumbani na Maisha ya elimu wanayo pitia .

Kupitia KKIISLAM BLOG mengi tutawaletea yanayo husu Wana AZHAR nchini Tanzania na Misri kwa ajili ya kufikia Malengo ya Maendeleo Insha Allah. 

Yakiwemo Historia ya kuanzishwa kwa Chuo Kikuu cha Azhar Shareef , Historia ya Umoja wa Wanafunzi wasomao Nchini Misri na Changamoto wanazo kutana nazo, Umoja wa Waliosoma Azhar Nchini Tanzania na Changamoto wanazo kumbana nazo, yote haya InshaAllah yatawajia karibu.
Tuwe pamoja.

No comments:

Post a Comment