Sunday, August 18, 2013

Miongoni mwa Sunna za Mtoto anapozaliwa ni kufanyiwa

Aqiyqah

kama alivyo tufundisha Mtume Muhammad (S.A.W) Rehma za M/Mungu zimshukie Juu yake na Amani na leo ndio ilikuwa Shughuli hiyo ya Mtoto wetu Salma M/Mungu akuze vyema yeye na watoto wote kwa Ujumla kila aina ya Mabala na Matatizo yawa epuke Mje Msimamie Dini ya M/Mungu InshaAllah.
Mtoto Salma . 

Aqiyqah ni jina lililopewa kichinjwa (mnyama) anaye chinjwa kwa mtoto mchanga aliyezaliwa awe ni wa kike au wa kiume.
 
    Ni Sunnah si waajibu / lazima . 

Dalili ya hili ni maneno ya Mtume (S.A.W) Rehma za M/Mungu zimshukie Juu yake na Amani  aliposema: "Atakayepata mtoto na akapenda amchinjie basi na afanye hivyo; kwa mwanamume mbuzi wawili na kwa mwanamke mbuzi mmoja".kama alivyosema Mtume.Hadith hii imepokewa na Maimaam Abuu Daawuud na An-Nasaaiy kutoka kwa ‘Abdullaah bin ‘Umar (Radhi za M/Mungu zimshukie Juu yake na Amani).

Kauli ya Mtume (S.A.W) Rehma za M/Mungu zimshukie Juu yake na Amani  aliposema“na akapenda amchinjie” ni dalili kuwa ‘Aqiyqah si lazima bali ni jambo linalopendeza Muislamu kulifanya. Lakini kwa mwenye uwezo wa kufanya hivyo basi iliyo bora zaidi kwake ni kufanya ama yule asiye na uwezo wa kufanya hivyo, basi si lazima kwake  maana Mwenyeezi Mungu Haikalifishi nafsi yoyote ila yale yaliyo sawa na uwezo wake na pia Hakufanya uzito katika dini.
Imethibiti kutoka kwa Mtume wa M/Mungu (S.A.W) Rehma za M/Mungu zimshukie Juu yake na Amani amesema: “Kila mtoto azaliwaye anafungamana na ‘Aqiyqah yake, anachinjiwa siku ya saba, ananyolewa kichwa chake na anapewa jina.” Wanachuoni wamelizungumzia neno ‘kufungamana’ hapa kuwa linaweza kuwa linamaanisha mambo mengi, miongoni mwa mambo hayo ni :-

A.Anakuwa kama mwenye kujisikia uzito na unyonge na mwenye kukosa wepesi na furaha maishani hadi achinjiwe.

B.Ni deni lililo mithili ya Rehani ambayo hulazimiana na mtu hadi alilipe.

Miongoni mwa Sharti kuu za chenye kuchinjwa    katika  ‘Aqiyqah kiwe kimesalimika na aibu mbalimbali kwa kifupi kabisa kichinjwa hichi kinafanana na kichinjwa cha ‘Eid Adhwhaa au Eid  kubwa.
WALIO HUDHURIA KATIKA HAFLA YA MTOTO WETU SALMA LEO .
Wageni walio hudhuria katika Shughuli hiyo .
Baba Mtoto Hussein Nassor Na Ustaadh Rajab Salum

No comments:

Post a Comment