Saturday, August 17, 2013

DINI NI NASIHA
Kutoka kwa Abu Ruqayyah Tamim Ibn Aus AddarryRadhi za M/Mungu zimshukie Juu yake  amesema kuwa Bwana Mtume Rehma za M/Mungu zimshukie Juu yake na Amani  kasema:
Dini ni nasiha.  Tukauliza: Kwa nani? Akasema kwa Allaah (Kukiri Uungu wake na kwamba Hana mshirika), Kitabu chake (Kukubali kuwa ni maneno ya Allah yasiyo na shaka), na Mtume wake (Kumkubali na kukubali ujumbe aliotumwa nao), na kwa Viongozi wa Waislamu (Kuwatii na kuwafuata katika mema na kuwaasa katika yale wanayokwenda nayo kinyume), na watu wa kawaida(kuusiana mema na kukatazana mabaya kwa njia nzuri).

Hadithi hii Imesimuliwa na Imamu  Muslim

No comments:

Post a Comment