Monday, July 29, 2013

KIFO NA UHAI NINI KIMETANGULIA KUUMBWA



M/Mungu Subhanahu Wataa3la anasema "Vipi mnamkanusha Mwenyezi Mungu na hali mlikuwa wafu akakufufueni! Kisha atakufisheni, tena atakufufueni, kisha kwake mtarejeshwa?."Qur an Suratul Baqara Aya ya 28.

M/Mungu kaanza Kutuumbia Kifo kisha Ukaumbwa Uhai Hii ni dalili kwamba tuishi Maisha yote ya Dunia lakini Siku ikifika Tutaiacha hii Dunia.

M/Mungu anasema tena katika Qur an " AMETUKUKA ambaye mkononi mwake umo Ufalme wote; na Yeye ni Mwenye uweza juu ya kila kitu.

Ambaye ameumba mauti na uhai ili kukujaribuni ni nani miongoni mwenu mwenye vitendo vizuri zaidi. Na Yeye ni Mwenye nguvu na Mwenye msamaha." Qur an Surat Al Mulk aya ya 1-2.

Ukiangalia Aya ya Pili utaona kuwa Mauti ndio Mwanzo kuumbwa kabla ya Uhai hii ni dalili ya kuwa Mauti yapo kama Mlango kuingia katika Mlango huo ni lazima.

Maandalizi mema ya Safari hii ni kufanya Matendo Mema ili kupata Radhi zake M/Mungu Pekee .

Mshairi Mmoja atukumbusha kwa kutwambia

LAU INGEKUWA DUNIA INABAKI MILELE NA WATU WAKE

BASI ANGE BAKI MTUME MUHAMMAD (S.A.W) YU HAI MILELE DAIMA.

Tujiandae na Safariii Ndugu zangu Wapendwa .

M/MUNGU ATUPE MWISHO MWEMA NA ATUKUTANISHE NA WAJA WAKE WEMA PEPONI SISI NA WAZAZI WETU NA WAISLAM WOTE KWA UJUMLA . AMIIN AMIIN AMIIN

No comments:

Post a Comment