Friday, August 09, 2013

MAMA SALMA AWATAKA WANAWAKE KUISHI MAISHA YA UPENDO.

Katika Kuwaaga Mwezi Mtukufu wa Ramadhani na kuingia Sikukuu ya Eid El Fitri Mama Salma Rashid Mke wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh Jakaya Mrisho Kikwete ametoa wito kwa Kina Mama Nchini  kuishi kwa Upendo , umoja na mshikamano hatua itakayosaidia kuimarisha hali ya amani na  utulivu.

Wito huo  umetolewa  na Mama Salma  wakati wa futari ya pamoja aliyoiandaa kwa ajili ya wanawake viongozi  na  wake wa viongozi  Ikulu jijini Dar es Salaam.

Mama Salma  alisema hakuna dini  hata moja inayowafundisha watu wake  kuishi maisha ya chuki bali dini zote zinasisitiza kuishi  kwa amani, umoja, na upendo jambo ambalo litamfanya binadamu aweze kumfikia  Mwenyezi Mungu.

“Bila ya kuangalia itikadi zetu tulizonazo,  sisi kama viongozi na wake wa viongozi tutumie nafasi tuliyonayo kuzungumza kwa vitendo  maneno matatu ya  upendo, amani na mshikamo ili jamii yetu iweze kuiga mfano kutoka kwetu”, alisema Mama Salma.

No comments:

Post a Comment