Saturday, August 17, 2013

NILICHOKUKATAZENI KIEPUKENI.

 Kutoka kwa Abu Hurayra  Abdur Rahman Ibn Sakhr Radhi za M/Mungu zimshukie Juu yake  alisema kuwa nimemsikia  Mtume  Rehma za M/Mungu zimshukie Juu yake na Amani  akisema:

Kile nilichokukatazeni kiepukeni, Na kile nilichokuamrisheni fanyeni kwa wingi kadiri muwezavyo. Hakika kilichowaangamiza watu wa Umma zilizopita, ni masuala (mahojiano) mengi na kupingana na Mitume yao.

Hadithi hii Imesimuliwa na Al-Bukhari na Muslim

No comments:

Post a Comment