Wednesday, August 14, 2013

TUKIO LA MBEYA SIKU YA EID LA KUPIGWA IMAMU

VIJANA Sita wilayani Kyela mkoani Mbeya wamefikishwa Mahakama ya Wilaya ya Kyela kujibu mashtaka manne wanayokabiliana kutokana na vurugu walizozifanya msikitini, ambapo Sheikh Mkuu wa Wilaya Kyela, Nuhu Mwafi lango na waumini wengine walipigwa na kuumizwa.
 
Tukio hilo lilitokea wakati wa Sikukuu ya Idiel- Fitr, wakati sheikh huyo akiongozwa swala. Wakisomewa mashtaka mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya Kyela, Joseph Luambano, ilidaiwa na Mwendesha Mashtaka wa Polisi, Nicholaus Tiba kuwa watuhumiwa hao wanakabiliwa na makosa manne. 


Ilidaiwa kuwa kosa la kwanza ni kula njama za kutenda kosa, kufanya vurugu msikitini, kufanya shambulio la kudhuru mwili na kujeruhi. Alidai kuwa siku ya tukio Sheikh Mkuu wa wilaya alishambuliwa akiwa anaendesha swala ambapo katika tukio hilo watu wengine, akiwemo mtunza hazina wa msikiti, Hamisi Hussein, alijeruhiwa kichwani.

Aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Ibrahimu shaban (17), Ambokile Mwangosi (19), Sadick Abudul (28), Mashaka Kassimu (30), Ahmed Kassimu (35 ) na Issa Juma (37). Alidai kuwa watuhumiwa hao wanakabiliwa na makosa hayo. Watuhumiwa wote walikana mashtaka wanayokabiliana nayo na upande wa mashtaka uliomba mahakama hiyo isiwapatie dhamana watuhumiwa ili wasivuruge ushahidi. Watuhumiwa walirudishwa rumande hadi hapo kesi yao itakapotajwa tena Agosti 26, mwaka huu ambapo shauri lao litasikilizwa tena

No comments:

Post a Comment