Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akiwa amepanda kwenye kivuko cha MV Musoma kinachovusha watu kutoka Wilaya ya Rorya na Musoma kikitokea Kinesi leo akielekea Musoma mjini tayari kwa kumalizia ziara yake mkoani Mara, ambapo amekagua miradi mbalimbali ya maendeleo na kuhamasisha wananchi kushiriki shughuli za maendeleo ikiwa ni pamoja na kukagua utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM, Kinana amemaliza ziara yake ya mikoa ya Shinyanga, Simiyu na Mara leo kwa kufanya mkutano mkubwa wa hadhara kwenye uwanja wa Mukendo mjini Musoma akiongozana na Katibu wa NEC Itikadi, Siasa na Uenezi wa CCM Nape N nauye.Ndugu Kinana amesema ni haki ya wananchi kuhoji maendeleo yao kwani wanasiasa wa vyama mbalimbali vikiwemo vya upinzani vilipita na kutoa ahadi tena wengine waliahidi kutoa asali na maziwa huku wengine wakiahidi wananchi kuwa wakiwachagua watajenga barabara za marumaru.
Msafara wa magari ukitoka kwenye kivuko cha MV Musoma mara baada ya kuwasili mjini Musoma leo ukitokea wilayani Rorya.
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM Ndugu Abdulrahman Kinana wa tatu kutoka kulia naKatibu wa NEC Itikadi, Siasa na Uenezi wa CCM Nape Nnauye wa pili kulia wakishuka kwenye kivuko cha MV Musoma mara baada ya msafara wake kuwasili mjini Musoma leo
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM Ndugu Abdulrahman Kinana na Katibu wa NEC Itikadi, Siasa na Uenezi wa CCM Nape Nnauye wakiwapungia mkiono wananchi waliojitokeza kuwapokea mjini Musoma
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akimsikiliza Jailos Chilewa Mhandisi mkazi wa mradi mkubwa wa maji wa ziwa Victoria uliopo Bukanga Makongo nje kidogo ya Manispaa ya Musoma wakati akitoa maelezo ya mradi huo, kutoka kushoto ni Katibu wa NEC Itikadi, Siasa na Uenezi wa CCM Nape Nnauye na Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Mara Bw. Christopher Sanya
Ukaguzi ukiendelea
Hii ndiyo ofisi yenyewe.
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akipokea zawadi jogoo kutoka kwamwenyekiti wa shina namba 6 mama ThabithaAmina Idd mara baada ya kutembelea shina hilo na kuongea na wanachama.
Katibu Mkuu wa Umoja wa wanawake UWT Mama Amina Makilagi akiwahutubia wana Musoma leo kwenye mkutano wa hadhara katika viwanja vya Mukendo mjini Musoma leo.
Hawa ni miongozi mwa wananchi waliohudhuria katika mkutano huo leo.
Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akizungumza na wana Musoma leo.
PICHA NA KIKOSI KAZI CHA FULLSHANGWE-MUSOMA MARA
No comments:
Post a Comment