Thursday, August 15, 2013

KUJA KWA JIBRIIL  KUWAFUNDISHA WAISLAMU MAMBO YA DINI YAO  
  
Kutoka kwa 'Umar Radhi za M/Mungu zimshukie Juu yake  amesema: Siku moja tulikuwa tumekaa na Mtume (S.A.W) Rehma za M/Mungu zimshukie Juu yake na Amani, Mara alitokea  mtu katika hiko kikazi ambacho tulichokaa ambaye  nguo zake zilikuwa nyeupe sana na nywele zake zilikuwa nyeusi sana; hakuwa na alama  ya machovu ya safari na wala hapakuwa na hata mmoja katika sisi aliyemtambua. Alienda akakaa karibu na Mtume (S.A.W) Rehma za M/Mungu zimshukie Juu yake na Amani, akaweka magoti yake karibu na magoti yake (Mtume) (S.A.W) Rehma za M/Mungu zimshukie Juu yake na Amani, na akaweka viganja vyake juu ya mapaja yake kisha akasema; Ewe Muhammad! Niambie kuhusu Uislamu.  Mjumbe wa Allaah alisema:  Uislamu ni kukiri kuwa hakuna mola isipokuwa  Allaah na Muhammad ni Mjumbe wake, kusimamisha Swalah, kutoa Zakaah, kufunga Ramadhaan na kwenda kuhiji (Makkah) ukiweza.  

(Akasema yule mtu yaani Jibriyl) Umesema kweli. Tulipigwa na mshangao kwa kumuuliza kwake Mtume (S.A.W) Rehma za M/Mungu zimshukie Juu yake na Amani, na kumsadikisha.  Na akasema tena: Niambie  kuhusu Imani. akasema Mtume (S.A.W) Rehma za M/Mungu zimshukie Juu yake na Amani Ni kumuamini Mwenyeezi-Mungu, Malaika Wake, Vitabu Vyake, Mitume Yake na siku ya Qiyaama, na  kuamini ya kuwa kheri na shari zinatoka Kwake M/Mungu Mtukufu .

Akasema Jibriyl: Umesema kweli, akasema hebu nielezee kuhusu Ihsani.  Akasema Mtume (S.A.W) Rehma za M/Mungu zimshukie Juu yake na Amani, Ni kumuabudu M/mungu Mtukufu    kama vile unamuona na kama humuoni basi Yeye Anakuona.  Akasema (Jibriyl):  Niambie    kuhusu Qiyaama.  Akajibu Mtume  (S.A.W) Rehma za M/Mungu zimshukie Juu yake na Amani, Muulizwaji si mjuzi kama vile Muulizaji (kwa Maana kwamba wewe Jibriyl ndiye Mjuzi zaidi kuhusu Qiyaama) . Kisha akamwambia: Nijulishe alama zake: Akajibu Mtume (S.A.W) Rehma za M/Mungu zimshukie Juu yake na Amani, Kijakazi atazaa bibi yake, na utaona wachunga wenda miguu chini, wenda uchi (wasio na uwezo wa kumiliki hata mavazi), mafukara (wasiokuwa hata na sehemu ya kuishi kwa umaskini) wakishindana kujenga majumba ya fahari. Kisha akaondoka (Jibriyl) na nilitulia kidogo (nikitafakari). Kisha akasema Mtume (S.A.W) Rehma za M/Mungu zimshukie Juu yake na Amani, "Ewe 'Umar! Je, unamjua ni nani yule aliyekuwa akiuliza? Nikasema: Allaah na Mjumbe wake wanajua zaidi.  Akasema Mtume   (S.A.W) Rehma za M/Mungu zimshukie Juu yake na Amani Ni Jibriyl, alikuja kuwafundisha dini yenu.

Imesimuliwa na Muslim.
-----------------------------------------------------------
 "مجىء جبريل ليعلم المسلمين أمر دينهم"
 عَن عُمَر رضي اللهُ عنه أَيْضاً قال:   بَيْنَما نَحْنُ جُلْوسٌ عِنْدَ رسُولِ الله صلى الله عليه وسلم ذات يَوْم  إذْ طَلَعَ عَلَيْنَا رَجُلٌ شَدِيدُ بَياضِ الثِّيَاِبِ شَديدُ سَوَادِ الشَّعْرِ، لا يُرَى عليه أَثَرُ السَّفَرِ ولا يَعْرِفُهُ مِنَّا أَحَدٌ، حَتى جَلَسَ إلى النَّبِّي صلى الله عليه وسلم، فأسْنَدَ رُكْبَتَيْهِ إلى رُكْبَتَيْهِ ووَضَعَ كَفَّيْهِ على فَخِذَيْهِ، وقال: يا محمَّدُ أَخْبرني عَن الإسلامِ، فقالَ رسُولُ الله صلى الله عليه وسلم:(( الإسلامُ أَنْ تَشْهَدَ أَنْ لا إلهَ إلا اللهُ وأَنَّ محمِّداً رسولُ الله، وتُقِيمَ الصَّلاةَ، وتُؤتيَ الزَّكاةَ، وتَصُومَ رَمَضان، وتَحُجَّ الْبَيْتَ إن اسْتَطَعتَ إليه سَبيلاً)). قالَ صَدَقْتَ. فَعَجِبْنا لهُ يَسْأَلُهُ ويُصَدِّقُهُ، قال : فَأَخْبرني عن الإِيمان. قال: ((أَن تُؤمِنَ باللهِ، وملائِكَتِهِ وكُتُبِهِ، ورسُلِهِ، واليَوْمِ الآخِرِ، وتُؤمِنَ بالْقَدَرِ خَيْرِهِ وشَرِّهِ)) قال صدقت. قال : فأخْبرني عَنِ الإحْسانِ. قال:(( أنْ تَعْبُدَ الله كَأَنَّكَ تَرَاهُ فإنْ لَمْ تَكُنْ تَرَاهُ فإنَّهُ يَرَاك)). قال: فأَخبرني عَنِ السَّاعةِ، قال: ((ما المَسْؤولُ عنها بأَعْلَمَ مِنَ السَّائِلِ )). قال: فأخبرني عَنْ أَمَارَتِها، قال:(( أن تَلِدَ الأمَةُ رَبَّتَها، وأَنْ تَرَى الحُفاةَ العَُراةَ العالَةَ رِعاءَ الشَّاءِ يَتَطَاوَلُونَ في الْبُنْيانِ )) ثُمَّ انْطَلَقَ، فَلَبِثْتُ مَلِيّاً، ثُمَّ قال : ((يا عُمَرُ، أَتَدْرِي مَنِ السَّائِلُ؟)) قُلْتُ: اللهُ ورسُولُهُ أَعلَمُ . قال:(( فإِنَّهُ جِبْرِيلُ أَتاكُمْ يُعَلِّمُكُمْ دِينَكُمْ))   
رَوَاهُ مُسْلِمٌ

No comments:

Post a Comment