Thursday, August 15, 2013

Sheikh Ponda : SIJUTII

SHEIKH Ponda Issa Ponda, Katibu wa Jumuiya na Taasisi za Kiislamu Tanzania, amesema hawezi kujutia harakati zake za kudai haki za Waislamu nchini licha ya misukosuko anayoipata kwa sasa. Anasema ikibidi yupo tayari kupoteza uhai wake.
“Natambua kwamba wapo wanaokerwa na harakati hizi, natambua wapo wanaojali harakati hizi bila kujali imani zao iwe ndani ya serikali ama nje ya serikali.

“Lakini kukwepa kusema ukweli ni kuahirisha vurugu nchini, nisiposema mimi wapo watakaosema kwa sauti kali kuliko yangu na wanaweza kuwa hatari (kama wanavyoniita) zaidi yangu tofauti na serikali inavyonitazama mimi, na hapo wajukuu zangu wataishi kwa wasiwasi zaidi,” Sheikh Ponda alimweleza mwandishi.

1 comment:

  1. Allah akupe shifaa njema. 2ponawe bega kwa dega

    ReplyDelete