Siku
moja baada ya ziara ya kushtukiza ya waziri wa uchukuzi Dk. Harison
Mwakyembe, kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini
Dar-es-Salaam, kiasi kikubwa cha dawa za kulevya kimekamatwa uwanjani
hapo katika harakati za kusafirishwa kwenda nchi za nje.
Dawa hizo aina ya Heroni kete 86 na bangi misokokoto 34 iliyokuwa ikisafirishwa na mtuhumiwa aliyetambulika kwa jina la Lenard
Jeremia Monyo,akiwa katika harakati za kuzisafirisha kwenda Italia
kupitia Zurich Uswis kwa shirika la ndege la Swiss Air, waziri Mwakyembe
amesema wafanyakazi wa mamlaka ya viwanja vya ndege na jeshi la polisi
kiwanjani hapo walimbaini mtuhumiwa huyo na kuahidi kufuatilia kesi hiyo
mpaka mwisho wake kwani haina haja ya upelelezi kwani kila kitu kipo
wazi.
Kuhusu kutaja majina na picha za watuhumiwa wa
usafirishaji wa dawa za kulevya kwenda nje ya nchi,waziri Mwakyembe
amesema kuwa, anasubiri kupata ushaidi na vielelezo vya majina na
picha,na kuwa kuanzia sasa wale wote watakao kamatwa na dawa za kulevya
picha zao zitachapishwa na kutangazwa kwenye vyombo vya habari ikiwemo
kilo 120 zilizokamatwa Afrika ya kusini.
Waziri Mwakyembe
amewaagiza viongizi wa mamlaka ya viwanja vya ndege kuona namna ya kuwa
zawadi vijana hao wa vyeo na kupandishwa mshahara jambo alilosema
atalifuatilia kuona utekelezaji wake,huku akidai kuwa watakaofanywa
vizuri watapongezwa na wale watakao haribu watafukuzwa kazi na
kufikishwa kwenye vyombo vya sheria,na kuwa wanaona utaratibu wa kuscan
mizigo yote inayopitia uwanja wa ndege na bandarini.
Awali
waziri Mwakyembe amesema kuwa hakuna mwenye uhakika na maisha yake kuwa
ana mkataba na Mungu alipoulizwa juu ya usalama wake kufuatia mtandao
huo kuwa mkubwa ambapo pengine unaweza kuhatarisha maisha yake,na
kuwataka idara zote zinazo husika na uwanjani hapo kushirikina kwa
pamoja katika kusafisha jina baya lililopata uwanja huo wenye kuwenzi
jina la baba wa taifa la Tanzania hayati Mwalimu Julius Kamabarage
Nyerere.
CHANZO: ITV
No comments:
Post a Comment