Monday, July 29, 2013

JE YAJUZU(INAFAA) KWA MWANAMKE KUKAA ITKAFU NYUMBANI KWAKE?

Moja katika Nguzo za itkafu ni Kukaa itkafu msikitini.
Hivyo iwapo kama Mwanamke atakaa itkafu Nyumbani kwake haito swihi kutokana na kukosekana Nguzo hiyo isipokuwa iwapo kama mwanamke atajetenga Nyumbani kwake na kujitahidi katika ibada Twatarajia atapata malipo makubwa insha Allah.

Iwapo mwanamke atahitaji kwenda kukaa itkafu msikitini yanahitajika mambo yafuatayo:

1.Kuwe msikitini kuna sehemu Maalum kwa wanawake.

2.Iwe ni sehemu yenye amani dhidi ya fitina kwa mwanamke huyu.

3.Ikiwa mwanamke kaolewa basi yatakiwa apate idhini kutoka kwa mumewe.

4.Isiwe katika kukaa kwake itikafu atapoteza haki za mumewe
wazazi wake au kulea watoto wake.

Tunamuomba M/Mungu azikubali Funga zetu na Maombi yetu yote kwa Ujumla ...

No comments:

Post a Comment