Monday, July 29, 2013

MAMBO YANAYO PENDEZA KUFANYWA NA MKAAJI WA ITKAFU

MAMBO YANAYO PENDEZA KUFANYWA NA MKAAJI WA ITKAFU

yafuatayo ni Baadhi ya Mambo yanayopendeza kwa Mwenye kukaa Itkafu kuyafanya .

1.Ibada za Sunna kama Vile Swala n.k
2.Kusoma Qur an
3.Kufanya Dhikri tofauti Mf, Tasbihi , Tahmid , Kuleta Takbir ,Istighfaar N.k
4.Kumswalia Mtume Muhammad (S.A.W) Rehma za M/Mungu zimshukie Juu yake na Amani.
5.Kukithirisha Kuomba Dua na Nyingi katika Ibada Ambazo hatuzazitaja hapa unazozifahamu.

Ni Jambo Jema Masheikh/Maustaadh katika Kipindi kama hiki cha Itkafu kukawa na Darsa katika Msikiti husika ili kupata Waumini kungeza Maarifa kwa kipindi kila ambacho wapo katika Ibada hiyo ya Itkafu.

Inapendeza kwa Mkaaji wa Itkafu achukue Vitu Muhimu atakavyo hitajia katika kipindi atakacho kuwa amejitenga / amekaa itkafu Msikitini ili asilazimike au aepuke kutoka toka Msikitini.

MAMBO YASIYO PENDEZA KUFANYWA NA MKAAJI WA ITKAFU
Haipendezi kwa mkaaji wa itkafu kujishughulisha na mambo yaliyo nje ya ibada na utiifu.Mfano mazungumzo yasiyo kuwa na faida na shughuli zisizokuwa na faida kwa mkaaji itkafu.Vile vile yachukiwa kwa mkaaji itkafu kukaa kimya na kuto zungumza akidhani ya kwamba hiyo ni katika ibada.

MAS A LLAH

JE YAJUZU(INAFAA) KWA MWANAMKE KUKAA ITKAFU NYUMBANI KWAKE AU MSIKITINI ?
InshaAllah endelea kufuatilia na tunakutakia Funga Njema ...

No comments:

Post a Comment