Monday, July 29, 2013

MUDA WA ITKAFU

MUDA WA ITKAFU

Muda wa itkafu ikiwa ni itkafu ya Wajib basi utatakiwa kukaa itkafu mpaka uishe ule muda Ulio Nadhiria kukaa itkafu.

Ama ikiwa ni itkafu ya sunna basi itkafu hii haina muda maalumu, bali Mja anapata Thawabu kulingana na muda atakao kaa msikitini.

MASHARTI YA ITKAFU

1.Uislam
2.Utambuzi
3.Twahara ya Janaba Hedhi na Nifasi.

Itkafu haiswihi kwa ASIYE kuwa Muislam wala mtoto asiyekuwa Mtambuzi Vile vile haiswihi kwa mwenye Janaba Hedhi na Nifasi.

NGUZO ZA ITKAFU

Kama tulivyo ieleza Maana ya Itkafu Kishaaria kuwa ni kukaa msikitini kwa nia ya kujikurubisha kwa M/Mungu Subhanahu Wataallah.

Kupitia Maana hiyo tunapata tambua kuwa Nguzo za Itkafu Ni

1.Nia ya kujikurubisha/Kumtii M/Mungu.

2.Kukaa msikitini.

Kwa Mujibu wa Nguzo hizo tulizo zitaja ikiwa Mtu atakaa Msikitini bila ya Nia ya Itkafu ya Kujikurubisha/Kumtii M/Mungu basi atakuwa hana Itkafu NDUGU KIJANA WA KIISLAM KUMBUKA KUWA NIA NDIO MPANGO MZIMA KATIKA IBADA ZETU ZETU ILI KUTOFAUTISHA KATI YA ADA NA IBADA NA HILI NDIO LENGO KUU LA NIA .

NAKUOMBA USINICHOKE TUENDELEE KUWA PAMOJA KATIKA MFULULIZO WETU HUU WA DARSA ZETU KUPITIA FACEBOOK ID :KIJANA WA KIISLAM DSM

UKURASA WA TUNAKUOMBA U - LIKE :Kijana wa Kiislam Tanzania
UKURASA WA TUNAKUOMBA U - LIKE :NAJIVUNIA KUWA BINT WA KIISLAM
WHATSAPP :+201110189580
SKYPE : al.amin_2010

Na : Ghalib N Monero L Azhary

No comments:

Post a Comment