Thursday, August 01, 2013

Wasifu wa Al-HABIB UMAR BIN AHMAD BIN ABI-BAKAR BIN SUMAYT AL, radhi za Mwenyezi Mungu zimwalie.

Bin Sumeit 2Si sisi wa kumweleza, hata ikasemwa kwamba kaelezwa. Letu sisi ni kurudi kwa wale ambao wanatambulika kwamba wanaweza kumzungumza.Nasi tumeamua kurudi kwa mwanazuoni wa wanazuoni wa zama zake na Bwana wa Msikiti Gofu na Ukutani na naibu wa al-Habib Umar bin Ahmad bin Abi-bakar bin Sumayt. Huyo ni Shaykh Sulayman bin Muhammad bin Said al-Alawy, radhi za Mwenyezi Mungu zimwaalie yeye na ma-Shekhe zake. Kwenye ijaza ndefu, anamwelezea hivi al-Habib:

“Na nimepokea riwaya ya ilmu vilevile kutoka kwa Bwana wangu na nguzo yangu, al-Habib, mwingi wa kuvumilia, mkuu aliyefika mbali kwenye ilmu, Imam, al-Allaama mtukufu, machomozo ya nuru za uwongofu, kiongozi wa ma-Imamu, na mwenye kuondosha mbabaiko, aliyekusanya ilmu za ndani na za nje mwenye wajihi unaopendeza, aliyetakasika na sifa zote chafu, mwenye akili inayowaka, Bwana wetu, Qutb, Umar bin Ahmad bin Sumayt al-Alawi radhi za Mwenyezi Mungu zimshukie. Nimemsahibu na nikatakhalaki kwa khuluka zake na mengine yake. Akanifanyia talqini ya dhikri. Na akanivisha na akanifanyia musaafaha na mushaabakah. Na ilbasi ilikuwa kwa juba la baba yake, Mwenyezi Mungu amrehemu. Na tena akanipa ijaza katika hayo. Na ningali bado nikienda kwake na yeye huyapamba masikio yangu kwa johari za hikma na hakika za irfaani njema kweli, ambazo ni nadra mtu kuzipata ama kuzisikia kwa asiokuwa yeye. Na kutoka kwake nimepokea riwaya ya baadhi ya kitabu cha al-Ihyaa kwa kusikiza na mimi kusoma mbele yake. Na vile vile baadhi ya vitabu vya ma-Bwana wakuu na vitabu vya ma-Bwana wa Bani Alawi. Na nimesoma kwake baadhi ya kitabu cha Tajriid as-Sahiih cha Hadithi. Akanipa ijaza kwenye vitabu thalathini na kitu vya fiqhi.”

No comments:

Post a Comment