Thursday, August 01, 2013

Wasifu wa Habib Ahmad Mash-hur

WASIFU AL-HABIB AS-SAYYID AHMAD MASH-HUR BIN TAHA AL- HADDAD, radhi za Mwenyezi Mungu zimwalie.

habib-ahmad-mashhur-haddadAl-Habib Ahmad Mash-hur.... al-Habib Ahmad Mash-hur. Ni jina lenye kutia ladha kinywani. Kama bwana wa Jailani, ambaye ana nasabu naye ya tarika na khirqa, bwana huyu alikuwa ni bwana wa shani. Si sisi wa kumweleza, hata ikasemwa kwamba kaelezwa. Letu sisi ni kurudi kwa wale ambao wanatambulika kwamba wanaweza kumzungumza.

Sheikh Suleiman Al-alawySisi tumeamua kurudi kwa mwanazuoni wa wanazuoni wa zama zake na Bwana wa Msikiti Gofu na Ukutani na naibu wa al-Habib Umar bin Ahmad bin Abi-bakar bin Sumayt. Huyo ni Shaykh Sulayman bin Muhammad bin Said al-Alawy, radhi za Mwenyezi Mungu zimwaalie yeye na ma-Shekhe zake. Kwenye ijaza ndefu, kamweleza hivi Habib Ahmad Mash-hur:

“Na katika wale ambao nimemshika miguu yake, nikanywa utamu wa mashrabu yake, al-Habib ambaye kakwea makweo ya kuhakiki mambo, akanywa shibe yake, ..... taa ya uongofu na mwenye kukwatua kutu za moyoni, mwana wa ma-Qutb na ma-Awtaadi na Ghawth wa miji na mawandani, mwanazuoni wa wanazuoni, mtukufu Ahmad Mash-hur bin Taha al-Haddad. Nimejumuika naye na nikaujaza moyo wangu pendo lake na nikapamba masikio yangu kwa johari za hikma zake, na nikamlazimu huku nachukua nuru za nasari yake na mashahiri yake na ikasihi kwangu kutokana na Habib huyu mapenzi yanayotokea kwa ajli ya Mwenyezi Mungu hata nikasiri mimi kuwa natajwa kwa jina la rafiki yake na mpenzi wake. Nataraji kwa Mwenyezi Mungu kuwa ataninufaisha naye hapa duniani na Akhera, pamoja na watoto wangu, na wapenzi wangu, na ndugu zangu, na wale waliotaalaki nami, na zitanirejea mimi baraka za Sayyid huyu adhimu, baraka za baba zake na wazee wake wa kale, na ambazo zitanipa mimi sifa za usahihi wa kuwa mimi ni Salman wao.”

                KWA MAKALA NYINGI ZAIDI TEMBELEA